Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen White

Sabato ni mada muhimu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato. Sio jambo la kushangaza, basi, kwamba Ellen G. White, mwanzilishi mwenza wa kanisa, alisoma mafundisho ya Biblia kuhusu Sabato na akaandika kiasi kikubwa kuhusu hilo.

Upendo wake kwa Yesu Kristo ndio uliomtia moyo kushika Sabato takatifu. Siku hii kuliko nyingine zote, alihisi karibu naye huku akikaribia familia yake na kuwahudumia wengine.

Basi, labda unajiuliza ni nini kilicho wafanya Waadventista Wasabato kama yeye kushika Jumamosi kama Sabato kwanza.

Unaweza kujiuliza Sabato za Ellen White zilikuwaje.

Au unataka tu kujua alichokiandika kuhusu siku hii maalum ya mapumziko.

Tutashughulikia:

Jinsi gani Ellen White alijifunza kuhusu Sabato ya siku ya saba?

Mwanzoni mwa mwaka wa 1846, Ellen Harmon mwenye umri wa miaka 18 (jina lake la kuzaliwa) na dada yake walimtembelea Joseph Bates, nahodha mstaafu na mfuasi mwaminifu wa kiadventista aliyekuwa ameanza kuweka Sabato. Alikuwa na hamu kubwa ya kuwasimulia ukweli aliokuwa amejifunza.

Hata hivyo, Ellen hakukubali Sabato ya siku ya saba mara moja, kulingana na maneno ya Joseph Bates. Badala yake, alikuwa mtunza Sabato baada ya miezi kadhaa alipokuwa amesadiki kuwa Sabato ya siku ya saba ni ya Kibiblia.

Familia ya Ellen walikuwa washiriki wa kanisa la Methodist na hivyo walishika siku ya kwanza ya juma (Jumapili), kama vile Waadventista wengine hapo awali mwanzo.

Kubadilika hadi kushika siku ya saba ilikuwa mabadiliko makubwa. Si ajabu kwamba jibu lake la awali lilikuwa la kusita sita.1 Aliandika:

“Sikuhisi umuhimu wake, na nilidhani kwamba [Bates] alikosea kwa kuzingatia amri ya nne zaidi ya zile tisa zingine.”2

Lakini alitamani kufuata Biblia na uongozi wa Roho Mtakatifu. hivyo , aliamua kuchunguza swala hili kwa undani.

Kujifunza kuhusu Sabato

The cover of the booklet Joseph Bates wrote on the Seventh-day Sabbath

Mwezi wa Agosti wa mwaka huo huo, Joseph Bates aliandika kitabu alichokiita Sabato ya Siku ya Saba—Alama ya milele. Alimpa nakala James White, mume wa Ellen, katika mazishi waliyohudhuria pamoja. James alikichukua nyumbani na wakakisoma kwa bidii. Ndani ya miezi michache, walikuja kuamini kuwa siku ya saba ilikuwa Sabato.

Hii hapa ni baadhi ya aya ambazo walisoma.

Kitabu kinaanza na Mwanzo 2:3:

“Mungu akaibariki siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya” (UV030).

Bates alisisitiza kuwa Sabato ilikuwepo tangu Uumbaji. Kwamba Ibrahimu alishika amri za Mungu (Mwanzo 26:5). Musa pia alitaja Sabato kama kitu ambacho Waisraeli walikuwa tayari wanajua kukihusu (Kutoka 16:23).

Baada ya kutazama Agano la Kale, Bates alionyesha maneno ambayo Yesu alisema kuhusu Sabato katika Agano Jipya.

Yesu alisema Sabato ilikuwa kwa ajili ya wanadamu wote, sio tu Wayahudi (Marko 2:27-28).

Hatimaye, Bates anathibitisha kwamba Amri Kumi, zilizoandikwa kwa kidole cha Mungu kwenye mawe (Kutoka 24:12), zilikuwa bado muhimu wakati wa Agano Jipya. Yesu alisema “… sikuja kutangua, bali kutimiliza” amri (Mathayo 5:17, UV030).

Bila shaka, Amri Kumi hizi zilijumuisha Sabato, ambayo ndio amri ya nne.

Wakati akisoma kitabu cha Joseph Bates, Ellen White pia alijifunza jinsi Sabato ilivyobadilishwa. Katika karne ya nne, mfalme Constantine—pamoja na Kanisa Katoliki—walibadilisha siku ya ibada kutoka siku ya saba hadi siku ya kwanza.

Aliandika:

“Hatungeweza kukubali neno la mwanadamu kwamba siku ya kwanza ilikuwa Sabato wakati Neno la Bwana lilisema siku ya saba ndiyo Sabato.”3

Kuamua kushika Sabato

Ellen na James White walianza kushika Sabato na kushiriki na wengine mwishoni mwa majira ya joto ya 1846. Mfano wao na ushauri wao uliwaongoza Waadventista wengi zaidi kwenye imani hiyo hiyo. Hatimaye, Sabato ya Kibiblia ilikuwa msingi wa imani wa Kanisa la Waadventista.

Lakini kuendelea kushika siku ya saba kama Sabato haikuwa jambo maarufu la kufanya, kwani madhehebu mengi ya Kikristo hushika Jumapili kama siku takatifu ya kwenda kanisani. Wana Sabato wapya walikabiliana na upinzani kwa sababu hiyo.

Hata hivyo, walibaki waaminifu kwa Mungu. Kwa upande wake, Mungu alihakikisha walikuwa wanafanya jambo sahihi kwa kumpa Ellen maono kuhusu Sabato.

Ni maono gani aliyokuwa nayo Ellen White kuhusu Sabato?

Ellen White alikuwa na maono kadhaa muhimu kuhusu Sabato.

La kwanza lilisaidia kuthibitisha hitimisho lake kwamba anapaswa kuitunza siku ya saba takatifu. Yaliyofuata yalishughulikia maelezo, kama vile jinsi inavyohusiana na unabii wa Biblia na matukio ya siku za mwisho, na wakati Sabato inaanza na kumalizika kila juma.

Lakini maono haya hayakutofautiana na Maandiko. Badala yake, yalithibitisha yale ambayo yeye na waamini wengine tayari walikuwa wakisoma katika Biblia.

Alihimiza umuhimu wa hili katika moja ya barua zake:

“Niliamini ukweli kuhusu swala la Sabato kabla sijaona chochote katika maono kuhusu Sabato.”4

Badala ya maono kumshawishi kuhusu ukweli, yalimsaidia kuuona umuhimu wa Sabato.

Maono kuhusu mwanga uliozunguka Sabato

Ellen White holding her arms up as she receives a vision

Ellen White alikuwa na maono mawili yanayofanana sana kuhusu Sabato mnamo Machi 6 na Aprili 3, mwaka wa 1847.5 Mara nyingi, maono haya hurejelewa kama maono ya “mzunguko wa Sabato”.

Aliona nini?

Katika maono, aliona hekalu la Mungu mbinguni. Chumba cha ndani, kinachoitwa Mahali Patakatifu Zaidi, kilikuwa na sanduku takatifu la agano (Ufunuo 11:19).

Ndani ya sanduku la agano kulikuwa nini?

“Niliona Amri Kumi zilizoandikwa kwa kidole cha Mungu. Kwenye kibao kimoja kulikuwa na nne, na kwenye kingine kulikuwa na sita. Zile nne kwenye kibao cha kwanza zilikuwa zinang’aa zaidi kuliko zile sita. Lakini ile ya nne, amri ya Sabato, iling’aa kuliko zote… Sabato takatifu ilionekana ya kushangaza – mng’ao wa utukufu ulikuwa ukiizunguka.”

Lakini kulikuwa na zaidi.

Alipelekwa kupitia mapitio ya mambo yanayotoa uhalali kwa Sabato na kuitunza.6

Aliona kwamba Sabato ingekuwa hoja ya maamuzi katika siku za mwisho. Watu wangelazimika kuchagua ikiwa watakuwa waaminifu kwa Mungu au kutii sheria za kidini za uwongo (Ufunuo 14:9–12).

Aliona kuwa wanaoshika Sabato wangepata mateso. Lakini bado kungekuwa na tumaini.

Baada ya mateso haya, Yesu angekuja na kuwachukua na kuwapeleka hadi Mji Mtakatifu atakapokuja kwa Mara ya Pili, ambao ulikuwa wazi kwa wale wanaoshika amri za Mungu (Ufunuo 22:14).

Sio kila kitu katika maono kilikuwa na maana kwa Ellen White, lakini alijua jambo moja: Kwamba,

“Maneno haya ya unabii yalipendekeza marekebisho ya Sabato.”7

Sabato na ujumbe wa malaika watatu

Wakati Ellen White alipata maono yake ya kwanza kuhusu Sabato, hakuelewa kila kitu alichokiona. Lakini masomo yake ya makini na maono mengine yalimsaidia. Algundua kwamba Sabato ilikuwa imefungamana na unabii muhimu wa siku za mwisho, hasa ujumbe wa malaika watatu katika Ufunuo 14.

Hapa kuna mapitio ya haraka ya ujumbe huo:

Malaika wa kwanza alitangaza hukumu ya Mungu na kuwaita watu waabudu Muumba (Ufunuo 14:6–7).

Malaika wa pili aliwasihi watu waache mchanganyiko wa kidini na mafundisho ya uongo ambayo Babeli inawakilisha (Ufunuo 14:8).

Lakini ujumbe wa tatu ukoje?

Ilikuwa ni onyo dhidi ya ibada ya uongo (Ufunuo 14:9–11). Na ililinganisha ibada hii na uaminifu wa watu wa Mungu:

“Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu na imani ya Yesu” (Ufunuo 14:12, UV030).

Ellen White na Waadventista wengine walipochunguza kifungu hiki katika Neno la Mungu, waligundua kuwa msingi wake ulikuwa ibada.

Wale wanaomsujudia Muumba (Ufunuo 14:7) watashika amri Zake—ikiwa ni pamoja na Sabato—badala ya kumwabudu “mnyama,” ambaye aliashiria mfumo wa dini ya uwongo.

Kwa maneno yake mwenyewe:

“Nilionyeshwa kwamba malaika wa tatu, akiihubiri amri za Mungu na imani ya Yesu, inawakilisha watu wanaopokea ujumbe huu na kuinua sauti ya onyo kwa ulimwengu, ili kudumisha amri za Mungu kama mboni ya jicho.”8

Maono kuhusu wakati wa Sabato

Kwa takribani miaka kumi, Waadventista wa Sabato walikubaliana juu ya wakati gani Sabato inapaswa kuanza. Mungu aliwaruhusu wawe na muda huu wa kuitafakari kutoka kwenye Biblia wenyewe kabla ya kumpa Ellen White maono ambayo yalithibitisha wakati sahihi wa kutatua swala hilo mara moja na kwa wote.

Joseph Bates aliamini kwamba Sabato inapaswa kuanza na kumalizika saa 12:00 jioni. Alikuwa na maoni kwamba hii ingesaidia kuepuka mkanganyiko wa nyakati za machweo ambazo zilikuwa tofauti kote ulimwenguni na kila mwaka. Wakristo Wengi wa Sabato—ikiwemo Ellen White—walishika Sabato kwa njia hii.9

Lakini wengine walidhani kwamba Sabato inapaswa kushikiliwa kutoka jua linapochomoza hadi jua linapochomoza. Wengine walipigania kuanzia machweo hadi machweo.

Ni ipi ilikuwa sahihi?

Mwaka wa 1847, Ellen White alipata maono kwamba imani ya kutoka jua kuzama hadi jua kuzama ilikuwa sio sahihi. Malaika alinukuu Mambo ya Walawi 23:32, ambayo inasema, “Tangu jioni hata jioni, mtaishika hiyo sabato yenu” (UV030).

Hata hivyo, haikuwa mpaka mwaka 1855 ndipo kila kitu kikawa wazi. Wakati huo, James White alimwomba J.N. Andrews, mmoja wa waadventista, kusoma kwa kina kuhusu somo hilo katika Biblia na kuandika jarida kuhusu hilo.

Hitimisho la Andrews?

Kulingana na Biblia, “jioni hadi jioni” ilimaanisha machweo hadi machweo. Ellen White alipokea maono muda mfupi baada ya hapo ambayo yalithibitisha hitimisho hili.10

Tangu wakati huo, Waadventista wa Sabato wameendelea kushika Sabato kutoka jua linapochwa Ijumaa hadi jua linapochwa Jumamosi.

Ellen White aliandika nini kuhusu Sabato?

Ellen White aliandika kwa wingi kuhusu Sabato, daima akirejea mafundisho ya Biblia kuhusu hilo. Anajadili:

  • Asili ya Sabato katika Uumbaji
  • Umuhimu wake
  • Utii wake katika historia
  • Uunganisho wake na unabii wa Biblia11
  • Kanuni za vitendo kwa ajili ya kushika Sabato

Maandishi yake yanazidi ukweli, ingawa.

Zinaeleza mpango wa awali wa Mungu kwamba Sabato ingekuwa siku ya mapumziko, furaha, uzuri, na kuungana naye.

Basi, tuonje kidogo.

Uumbaji na Umuhimu wa Sabato

Maandiko ya Ellen White mara nyingi huzungumzia sababu za Mungu kutoa Sabato kama baraka kwa wanadamu. Mambo yake muhimu ni:

  • Mungu alitoa Sabato wakati wa Uumbaji.
  • Inakumbusha kwamba Mungu ndiye Muumba wetu.
  • Ni ishara ya jinsi Mungu anavyotufanya watakatifu.
  • Inakuza uhusiano wetu na Mungu.

Hivi ndivyo anavyounganisha Sabato na Uumbaji: “Ilikuwa kumbukumbu ya kazi ya uumbaji, na hivyo ishara ya uwezo wa Mungu na upendo wake.”12

Mahali pengine, aliandika,

“Kwa kushika Sabato ya kweli, Wakristo wanapaswa kuushuhudia ulimwengu kwa uaminifu ufahamu wao wa Mungu wa kweli na aliye hai tofauti na miungu bandia yote, kwa kuwa Bwana wa Sabato ndiye Muumba wa mbingu na nchi.”

Mbali na kuwa kumbukumbu ya Uumbaji, Sabato ni ishara ya kile Mungu anataka kufanya maishani mwetu. Ukirejelea Ezekieli 20:12, Ellen White anasema, “Sabato ni ishara ya nguvu ya Kristo kutufanya watakatifu.”13

Pia ni “ishara ya uhusiano uliopo kati ya Mungu na watu wake.”14 Kwa maneno mengine, Sabato ni kuhusu ukuaji wa kiroho.

Baada ya yote, Mungu aliifanya Sabato kwa ajili yetu:

“Mwanadamu hakuumbwa ili apaswe Sabato; kwa maana Sabato iliundwa baada ya uumbaji wa mwanadamu, ili kukidhi mahitaji yake.”15

Hakutupatia Sabato kama kigezo cha orodha ya kidini (Marko 2:27-28). Alikuwa anataka iwe siku ambayo tunaweza kuepuka shinikizo za kila siku na kuimarisha uhusiano wetu naye – kupitia sala, ibada, kusoma Biblia, muda na watu, na kuwahudumia wengine.

Tunaposhiriki Sabato na mtazamo huu, tunapata amani na mapumziko katika Yesu (Mathayo 11:28–30). Maandishi ya Ellen White yanadokeza uzoefu mzuri huu.

Sabato kupitia historia

Ellen White anaandika jinsi waamini waaminifu walivyoitunza Sabato katika historia.

Anatoa ushahidi kutoka kwenye Biblia kwamba kutunzwa kwake kunaanzia nyuma sana kama uumbaji, Wazee—Nuhu, Ibrahimu, n.k.—walishika Sabato. Pia anafuatilia uzoefu wa Waisraeli katika kushika Sabato hadi wakati wa Yesu.

Katika kitabu chake juu ya maisha ya Kristo,16 anachambua kwa undani mamlaka Yake juu ya Sabato. Hakuja kuondoa sheria. Badala yake, alikuja kuitimiza na kuifanya iwe huru kutoka kwa vizuizi vyote vilivyowekwa na wanadamu, kama vile Mafarisayo.

Zaidi, anasisitiza jinsi Kristo alivyoshika Sabato:

  • Aliponya wagonjwa.
  • Alihudhuria masinagogi na kufundisha huko.
  • Alijipatia muda katika asili.

Kazi yake muhimu, Pambano Kuu, inachunguza jinsi Sabato ilivyobadilishwa kuwa Jumapili na Kanisa Katoliki wakati wa karne ya nne (ambayo imeandikwa katika katekisimu yake). Licha ya hivyo, kundi dogo la watu wakati huo liliendelea kushika Sabato. Na mwishoni mwa nyakati, kabla Yesu arudi wakati wa Kuja Kwake mara ya Pili, Sabato itakuwa kama muhuri unaotofautisha wafuasi waaminifu wa Mungu.17

Mara nyingi anataja Isaya 58:12–14 kuonyesha kwamba watu wa Mungu watarudisha umuhimu wa Sabato. Hapa kuna kipande:

“Uvunjaji ulifanyika katika sheria ya Mungu wakati Sabato ilipobadilishwa…. Lakini wakati umefika kwa taasisi hiyo takatifu kurudishwa. Uvunjaji huo unapaswa kurekebishwa.”18

Watu wa Mungu watarejesha kushika Sabato ya kweli wanapotangaza ujumbe wa malaika wa tatu, ambao ni mwito wa kushika amri za Mungu na imani ya Yesu.19

Ingawa Ellen White aliandika mengi kuhusu upande wa theolojia wa Sabato, pia alitoa ushauri wa vitendo. Tutachunguza hilo baadaye.

Kulinda Sabato takatifu

Wakati Waadventista walipokuwa wanajifunza kuhusu Sabato kwa mara ya kwanza, walijiuliza jinsi ya kuitunza kulingana na amri ya Mungu (Kutoka 20:8). Ellen White aliwasaidia kukidhi mahitaji haya kwa kuandika kuhusu kanuni za Kibiblia za kutunza Sabato takatifu, kama vile:

  • Kutumia Ijumaa kama siku ya maandalizi kwa Sabato
  • Kuepuka kazi zisizo za lazima
  • Kutenga mambo yote ya kidunia ili kumtazama Mungu
  • Kumwabudu Mungu pamoja kanisani
  • Kutumia muda kusoma Biblia au kutembea katika asili
  • Kutumikia wengine
  • Tuzame katika haya.

Katika Biblia, Waisraeli waliandaa chakula chao na kumaliza kazi zao kabla ya Sabato (Kutoka 16:23; Hesabu 11:8). Anatumia kanuni hii kwetu:

“Ijumaa acha maandalizi ya Sabato yakamilike. Hakikisha kuwa nguo zote ziko tayari na kwamba upishi wote umekamilika.”20

Kwa njia hii, Sabato inaweza kuwa wakati wa kumkaribia Mungu zaidi. Kazi isiyo ya lazima inaweza kuepukwa:

“Hii inapaswa kuwa siku ya baraka kwetu – siku ambayo tunapaswa kuweka kando mambo yetu yote ya kidunia na kuweka fikira zetu katika Mungu na mbinguni.”21

Tazama sehemu ya kwanza

Sabato imekusudiwa kuwa baraka! Mara nyingi, Ellen White anasisitiza furaha na raha yake. Alisema familia nzima inaweza kutarajia siku hiyo zaidi ya siku nyingine yoyote.22

Moja ya mambo muhimu ya Sabato ni ushirika na waamini wengine. Wakati mmoja, Ellen White alizungumza na mwanamke ambaye alidhani angevunja Sabato ikiwa angechukua usafiri wa umma kwenda ibada ya Sabato.

Hili lilikuwa jibu la Ellen White:

“Nilimwambia hapana; kwamba ilikuwa ni machukizo kwa Mungu kubaki mbali na mikutano kuliko kusafiri kwa gari ili kukutana pamoja kuabudu Mungu.”23

Shule ya Sabato, kama shule ya Jumapili, ilikuwa sehemu ya mikutano hii. Ilikuwa na madarasa kwa watu wa umri tofauti kusoma Biblia pamoja. Aliandika sana kuhusu shule ya Sabato hivi kwamba kitabu kamili kimeandikwa na ushauri wake kuhusu hilo.24

Kuhusu shughuli za Jumamosi mchana, anahimiza wazazi kutumia muda na watoto wao badala ya kuwaacha watoto wenyewe. Wanaweza kufanya mambo pamoja, kama vile kusoma hadithi za Biblia au kuwapeleka nje katika asili ambapo wanaweza kufurahia uumbaji wa Mungu.25

Pia anatumia mfano wa Yesu katika Mathayo 12:12 kuonyesha kwamba Sabato ni siku ya kubariki wengine na “kupunguza mateso.”

Baada ya kusoma baadhi ya maagizo haya, unaweza kujiuliza jinsi Ellen White alivyoitunza Sabato.26

Soma ili upate kuchunguza mazoezi yake mwenyewe.

Jinsi gani Ellen White alitunza Sabato?

Kwa Ellen White, Sabato ilikuwa siku ya thamani pamoja na Yesu na familia yake. Daima alifanya bidii yake kujiandaa kwa Sabato ili asiwe na haja ya kufikiria kazi au biashara mara Sabato ilipoanza. Mara kwa mara, familia yake ingehudhuria ibada kanisani na kisha kutumia muda pamoja mchana. Nyakati nyingine, yeye na mumewe walikuwa na majukumu ya kuhutubia ambapo walikuwa wanawatia moyo na kuwasaidia watu.

Yafuatayo yalikuwa maneno kwenye jarida lake ikionyesha umuhimu wa siku ya Sabato kwake:

“Tulijinyenyekeza mbele za Mungu mwanzoni mwa Sabato. Nikaanza kuomba na moyo wangu ukamtafuta Mungu…. Yesu alionekana mwenye thamani sana, sana kwangu. Niliweka mizigo yangu yote kwa Mwokozi wangu na nikapata faraja.”27

Haya ni baadhi ya maneno aliyotumia kuelezea Sabato:

  • “Furaha”
  • “Baraka”
  • “Siku yenye thamani kuu”
  • “Siku maalum ya kufunga na kuomba”
  • “Masaa yenye amani”

Hebu tuangalie jinsi Sabato ya kawaida ingeweza kuonekana nyumbani kwa familia ya White.

Kutumia Sabato pamoja na familia yake

Ellen White and her family as they celebrate weekly Sabbath together.

Courtesy of the Ellen G. White Estate, Inc.

Kwa familia ya White, furaha ya Sabato ilianza wakati wa machweo siku ya Ijumaa jioni walipotumia muda katika maombi, ibada, na kuimba.

Asubuhi iliyofuata, familia ingeamka mapema ili “waweze kwenda ibadani bila haraka wala wasiwasi.”28

Kwanza, walihudhuria shule ya Sabato, ikifuatiwa na ibada kuu.

Siku za Sabato, Ellen White angeandaa chakula cha haraka mapema kwa ajili ya familia kula. Mkaza mwanawe anaeleza:

“Kazi zote zisizo za lazima ziliachwa kufanywa siku ya Sabato lakini kamwe Bi. White hakufikiria kuwa ni uvunjaji wa kufuata Sabato ipasavyo kutoa huduma za kawaida za maisha, kama vile kuwasha moto kwa ajili ya kupasha moto nyumba au kuandaa chakula kwa ajili ya milo.”29

Mchana, familia mara kwa mara walikuwa wakichukua mapumziko nje ili kufurahia asili.

Kusoma pamoja ilikuwa moja ya shughuli zao za Sabato. Msaidizi katika nyumba yao alisema kwamba Ellen White “alitumia muda mwingi kusoma na [watoto wake] siku ya Sabato kutoka kwenye uteuzi wake mkubwa wa vifaa vya kimaadili na kidini.”30

Machweo yalipofika, familia ingekusanyika tena kwa ibada.

Kuhudumia wengine siku ya Sabato

Ellen White hakuwa nyumbani siku za Sabato kila wakati kutokana na safari nyingi walizokuwa nazo yeye na mumewe.

Hivi ndivyo shughuli za huduma zao zingeweza kuonekana wakati huo:

  • Kuzungumza katika ibada au mikutano inayoitwa makambi
  • Kutembelea watu kuwashauri na kuwatia moyo
  • Kusali na kuwajali wagonjwa
  • Kusafiri kwenda kwenye mikutano ya kuzungumza (ingawa walijaribu kuepuka safari kama ingewezekana)31

Kwa mara kadhaa, wangefanya Sabato tulivu kama alivyoelezea katika jarida hili:

“Tulikuwa na siku nyingine nzuri…. Tulichukua uandishi wetu na kutembea umbali mrefu kufikia kivuli cha mti ili kupata mahali tulivu pa kuandika…. Tulikula chakula chetu cha mchana chini ya mti.”32

Kupitia maisha yake yote, Ellen White alilinda Sabato katika maandishi yake na mfano wake. Alichukulia thamani kwa sababu ilikuwa siku—kuliko nyingine yoyote—ambapo alikaribia sana na Yesu na kufanya kazi pamoja Naye.

Gundua baraka za Sabato kwa ajili yako

A person sitting on a bench at seashore looking at sunset at the horizon, as we discover blessings of Sabbath for ourselves.

Photo by Sid Leigh on Unsplash

Tumepata taswira ya Sabato na uzuri wake kupitia macho ya Ellen White. Na kila wakati, tumegundua kuwa Biblia ndio msingi.

Maono yake kutoka kwa Roho Mtakatifu kuhusu Sabato yalisaidia yeye na Waadventista wa mwanzo kujua kwamba walikuwa wakielekea upande sahihi. Lakini hayakuwa yakiwaambia chochote ambacho Biblia haikuwa tayari imekwisha kusema. Yalimsaidia kutumia yale ambayo Roho Mtakatifu alikuwa akimfundisha alipokuwa akisoma Biblia.

Na Biblia ndiyo sababu ya Waadventista kushika Sabato leo.

Sabato ni amri, kanuni, na baraka ya Kibiblia, inayotualika kwenye mkutano maalum na Mungu ambapo tunaweza kuacha kazi na kuzingatia kuimarisha uhusiano wetu naye. Hivyo, tunashika siku ya Sabato kuwa takatifu kwa upendo wetu kwake na hamu yetu ya kuwa karibu naye—sawa na jinsi Ellen White alivyofanya.

Kama umesoma kuhusu furaha ya Sabato na umuhimu wake kwa wafuasi wa Mungu katika siku za mwisho, ungependa kujifunza zaidi?

  1. Coon, Roger W., A Gift of Light, (1998), p. 25. []
  2. Rebok, Denton Edward, Believe His Prophets, (1955), p. 76. []
  3. White, Ellen G., Letters and Manuscripts, vol. 2, Letter 12, 1869. []
  4. White, Ellen G., Letters and Manuscripts, vol. 2, Letter 2, 1874. []
  5. Maxwell, Mervyn, Tell It to the World (Pacific Press, Nampa, ID, 1977), p. 92. []
  6. White, A. L., Ellen G. White: The Early Years: 1827–1862, vol. 1 (Hagerstown, MD, Review and Herald, 1985), p. 121. []
  7. White, Ellen G., Testimonies for the Church, vol. 1 (Mountainview, CA: Pacific Press, 1948), p. 78. []
  8. Ibid., p. 77. []
  9. Douglass, Herbert, Messenger of the Lord, (Pacific Press, Nampa, Idaho, 1998), p. 156. []
  10. White, Ellen G., Testimonies for the Church, vol. 1, (Mountainview, CA: Pacific Press, 1948), p. 116. []
  11. White, Ellen G., White Topical Index, “Sabbath.” []
  12. White, Ellen G., The Desire of Ages (Pacific Press, Mountain View, CA, 1898), p. 281. []
  13. Ibid., p. 288. []
  14. White, Ellen G., Counsels on Health (Pacific Press, Mountain View, CA, 1923), p. 358. []
  15. White, Ellen G., Testimonies for the Church, vol. 2 (Pacific Press, Mountain View, CA, 1868), p. 582. []
  16. White, Ellen G., The Desire of Ages (Pacific Press, Mountain View, CA, 1898), pp. 281–289. []
  17. White, Ellen G., The Great Controversy (Pacific Press, Mountain View, CA, 1911), p. 605. []
  18. Ibid., p. 452. []
  19. Ibid., p. 453. []
  20. White, Ellen G., Child Guidance (Review and Herald, Washington D.C., 1954), p. 528. []
  21. Ibid., p. 529. []
  22. Ibid., p. 531; The Great Controversy (Pacific Press, Mountain View, CA, 1911), p. 536. []
  23. White, Ellen G., The Ellen G. White 1888 Materials (Ellen G. White Estate, Washington, D.C., 1987), p. 773. []
  24. White, Ellen G., Testimonies on Sabbath-School Work. []
  25. White, Ellen G., Child Guidance, p. 533; White, Ellen G., “Never Yield the Sabbath,” Signs of the Times, Feb. 28, 1878. []
  26. White, Ellen G., Selected Messages, book 3 (Review and Herald, Washington D.C., 1980), p. 258. []
  27. White, Ellen G., Letters and Manuscripts, vol. 2, Letter 7, 1876. []
  28. White, Ellen G., Sermons and Talks (Ellen G. White Estate, Silver Spring, MD, 1994), p. 107. []
  29. White, Ellen G., Selected Messages, book 2 (Review and Herald: Washington D.C., 1958), p. 263. []
  30. White, Ellen G., An Appeal to the Youth (SDA Publishing Association, Battle Creek, MI, 1864), p. 19. []
  31. White, Ellen G., Letters and Manuscripts, vol. 2, Manuscript 13, 1873. []
  32. Ibid., Manuscript 8, 1873. []

Je, Una swali kuhusu Waadventista? Uliza hapa!

Pata majibu kwa maswali yako kuhusu Waadventista Wasabato

Majibu Zaidi

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. White

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. White

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. WhiteEllen G. White ni jina linalojulikana sana miongoni mwa Waadventista wa Sabato, lakini pia aliathiri sehemu nyingi za historia, mbali na kuwa mwanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Ndiyo maana Jarida la Smithsonian...

Wafahamu Watoto wa Ellen White

Wafahamu Watoto wa Ellen White

Ellen White, ambaye ni mmoja wa waanzilishi maarufu zaidi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, alikuwa na watoto wanne na mumewe, James: Henry Nichols, James Edson, William Clarence, na John Herbert.

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa Waadventista

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa Waadventista

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa WaadventistaWaadventista wa Sabato wanajulikana kwa kusisitiza maisha yenye afya bora. Na Ellen G. White alikuwa na ushawishi mkubwa katika maendeleo ya kipaumbele hiki na utekelezaji wake miongoni mwa Waadventista....