Jinsi Biblia Inavyotafsiri Upendo

Kila mtu anazungumza kuhusu upendo, lakini je tunajua maana yake halisi?

Upendo leo unaonekana kuwa… wa bei rahisi sana. Wanandoa wanakiri upendo wao kwa kila mmoja, na baada ya miaka (wakati mwingine miezi!), wameachana au kupeana talaka. Yawezekana mtu katika maisha yako alidai kuwa anakupenda na bado akakutumia na kukudanganya.

Au, hata kama hawakukusaliti au kukudhulumu moja kwa moja, labda mambo yalionekana kuwa upande mmoja, kana kwamba hawakujali sana kuhusu kuweka juhudi katika uhusiano wenu.

Je huu ndio upendo ambao tunasema Mungu anao?

Haiwezekani.

Jambo la kushukuru ni kwamba, Biblia inatupatia picha tofauti ya upendo—sio wa maneno matupu na hisia zisizo na kina bali ni matendo ya kweli ya upendo na hisia adhimu zinazochochewa na uamuzi. Mungu Mwenyewe anajumuisha upendo huu, akionyesha jinsi upendo unavyotoa na kujitoa mhanga kwa ajili ya mwingine.

Kadri tunavyofunua picha hii, unaweza kutarajia kujifunza:

Huenda ukagundua kwamba upendo ni tofauti sana na ulivyo fikiria—na zaidi.

Upendo ni nini kulingana na Maandiko?

A cross, representing God's love for us in giving Jesus to die

Photo by il vano on Unsplash

Upendo, kama ulivyo elezwa katika Biblia, ni wa kujitolea na usio na masharti, ukilenga kile kilicho bora kwa mwingine na kutoa uhuru wa kuchagua ikiwa tutapenda pia. Mungu Mwenyewe alionyesha upendo huu kwa kumtoa Yesu Kristo afe kwa ajili ya dhambi za ulimwengu (Yohana 3:16; Warumi 5:6-8). Alitoa kwa kujitolea na bila masharti, lakini hamlazimishi mtu yeyote kupokea zawadi hii; anaturuhusu kuchagua ikiwa tutaitikia.

Maelezo wazi zaidi ya upendo huu yapo katika 1 Wakorintho 13. Sura hii inatupa wazo la upendo wa kweli ni nini na nini sio. Hebu tuangalie:

1 Wakorintho 13 (UV030)
Upendo Ni Nini Nini Sio Upendo
Huvumilia Wivu
Hufadhili Kujisifu
Hufurahi pamoja na kweli Ujeuri
Huvumilia yote Ukali
Huamini yote Kusisitiza njia yake mwenyewe
Hutumaini yote Kukasirika
Hustahimili yote Kuwa na chuki
Haupungui neno wakati wo wote Kufurahia maovu

Neno moja linalohitimisha sifa zote za tabia hizi ni kujitolea. Na linazidi maneno:

“Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli” (1 Yohana 3:18, UV030).

Hivi ndivyo upendo unavyoonekana kulingana na Neno la Mungu:

  • Kuhudumiana (Wagalatia 5:13)
  • Kufanya kilicho bora kwa mwingine (Warumi 13:10)
  • Na hata kutoa maisha yake kwa ajili ya mwingine (Yohana 15:13)

Haya yote yanaweza kufupishwa katika Amri Kumi, ambazo hutoa kanuni za kumpenda Mungu na kupendana sisi kwa sisi:

“Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” (Mathayo 22:37-40, UV030).

Amri Kumi zinaeleza maana ya upendo, na tunapompenda Mungu, itakuwa ni jambo la kawaida kwetu kutaka kuzifuata (1 Yohana 5:3; 2 Yohana 1:6).

Kwa namna ile ile, dhambi na ubinafsi ni kinyume cha upendo huo kwa sababu inavunja sheria (1 Yohana 3:4). Ikijumuisha tabia kama uzinzi, mauaji, wizi, kutamani, na chuki kwa wengine (1 Yohana 4:19-21).

Habari njema kuhusu sheria hii ni kwamba husaidia kuweka mipaka inayoeleweka kuhusu upendo. Kumpenda mtu hakumaanishi kwamba kila kitu kinakubalika katika uhusiano. Mara nyingine, jambo la upendo zaidi ni kutoruhusu tabia zisizofaa (Methali 3:12), iwe ni unyanyasaji wa kihisia au kimwili, udanganyifu, kudanganya, au zaidi.

Mtaalam wa theolojia Jiri Moskala, ThD, anasisitiza upande huu wa upendo:

“Upendo pia ni mgumu: Hautavumilia dhambi, chuki, ubinafsi, na kiburi; kwa mtazamo huo, ni wa kipekee. Upendo imara na wenye afya huelewa lakini haukubaliani na udhalimu na aina nyingine za uovu.”1

Na kama tulivyotaja, sehemu muhimu ya upendo wa Kibiblia ni uhuru. Mtu mwenye aina hii ya upendo atatambua kwamba watu wana uhuru wa kukubali au kukataa upendo huo.

Upendo huu unaonekana tofauti na tunavyoona mara nyingi. Lakini ndio unafanya mahusiano kuwa salama na yenye afya.

Aina za upendo katika Biblia ni zipi?

Lugha ya Kiingereza ina neno moja tu linaloeleza upendo, lakini Kigiriki hutumia maneno mengi—mengi ya hayo huonekana katika Agano Jipya. Maneno muhimu, kwa Kiingereza, ni upendo wa kujitoa kafara, upendo wa ndugu, upendo wa kujipenda, na upendo wa kimapenzi. Makundi haya yanaweza kutusaidia kuelewa zaidi kuhusu upendo wa Mungu.

Tutaangalia kwa kifupi kila moja na jinsi zinavyoonekana katika Biblia.

Agape

A sister showing unselfish love by giving her brother a hand after he fell

Photo by Annie Spratt on Unsplash

Agape ni neno la Kigiriki linalomaanisha upendo usio na masharti, wa kujitoa kafara na usio na ubinafsi. Ni upendo unaotegemea kanuni, na ni “hasa kazi ya kichwa, fikra, na akili.”2

Hii ni aina ya upendo ambao huchagua kufanya kilicho bora kwa mtu mwingine, hata wakati huenda hujisikii kufanya hivyo. Inazidi hisia au mvuto.

Hapa kuna mifano michache katika Biblia:

“Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi” (Mathayo 5:44, UV030).

“Twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza” (1 Yohana 4:19, UV030).

Upendo wa ndugu

Phileo ni upendo kati ya ndugu au urafiki. Ni “zaidi swala la moyo, hisia.”3 Baada ya yote, kawaida unakuwa rafiki na mtu kwa sababu unafurahia kuwa nao na kuhisi karibu nao. Hauhitaji kuwa karibu nao lakini unataka kuwa.

Ni aina ya upendo ambao Yesu alikuwa nao kwa rafiki yake Lazaro (Yohana 11:3). Neno hilo pia hutumiwa kuelezea upendo ambao waamini katika Kristo wanatakiwa kuwa nao kila mmoja kwa mwenzake (Tito 3:15).

Maneno mengine ya Kigiriki yanahusiana kwa karibu sana na hili:

  • Philoxenia: ukarimu au upendo kwa wageni (Warumi 12:13; Waebrania 13:2)
  • Philostorgos: upendo, hasa kati ya ndugu au wanafamilia (Warumi 12:10)

Philautia (Upendo binafsi)

Two young women pursing their lips and posing for a selfie showing self love

Photo by Andrea Piacquadio

Philautia inaweza kumaanisha upendo wa kujipenda au kujipenda kupita kiasi.

Aina ya kwanza—kujipenda—sio wa kibinafsi.

Kwa kweli, ni wa kibiblia. Yesu anatuita kuwapenda jirani zetu kama tunavyojipenda wenyewe (Mathayo 22:39). Hii inahusisha kutambua thamani yetu na kujitunza jinsi Mungu alivyotuumba ili tuweze kutumikia wengine kwa ufanisi zaidi.

Kujipenda kupita kiasi, hata hivyo, ndio tunachokiona katika aya kama 2 Timotheo 3:2, ambayo inaelezea tabia za watu katika siku za mwisho: “wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi” (UV030).

Ingawa neno mpenzi hutumiwa kuelezea watu ambao “wanapenda nafsi” au “wanaopenda fedha,” hii ni mbali na maana ya upendo tunaoelezea katika makala haya. Kupenda kupita kiasi na kulazimisha sio upendo, ingawa wanaweza kuonekana hivyo.

Eros

Eros ni neno la Kigiriki linalomaanisha upendo wa kimapenzi au wa kingono (usichanganywe na tamaa, ambayo ni ya kibinafsi).

Neno lenyewe halitumiki katika Biblia, ingawa tunaona mifano yake. Mifano yenye kuonekana zaidi iko katika Wimbo Ulio Bora, ambapo upendo wa kimapenzi wa kina unatajwa:

“Kubusu na anibusu kwa kinywa chake. Maana pambaja zako zapita divai….Nivute nyuma yako, na tukimbie” (Wimbo Ulio Bora 1:2, 4, UV030).

Upendo wa Mungu ni upendo wa aina gani?

A pair of glasses and the Scrabble letters l-o-v-e sit on an open Bible.

Photo by Emmanuel Phaeton on Unsplash

Wakristo wengi wanautambua upendo wa Mungu kama ule wa kujitolea, wenye kanuni, unaoleta uhuru uitwao agape. Na bila shaka, ni hivyo. Hata hivyo, Biblia pia inazungumzia upendo wa Mungu kama phileo. Na ukifikiria kuhusu hilo, je, si kila aina ya upendo safi na wa kweli unatuonyesha Mungu ni nani?

Hata hivyo, hebu tuanze na agape.

Biblia inatuambia kwamba “Mungu ni upendo [agape]” (1 Yohana 4:8, UV030).

Mchungaji Ty Gibson anabainisha kwamba aya hii ni “kielelezo pekee cha jumla cha utambulisho” kuhusu Mungu katika Biblia.4 Haijasema, “Mungu ni mwenye upendo.” Badala yake, Mungu ni upendo katika kiini chake. Na ili kuwakilisha upendo huu kamili , Mungu ni uhusiano hai—Utatu. Utatu ni “picha ya Mungu kama umoja wa upendo kamili wa pande tatu.5

Fikiria kwa namna hii:

Bila mtu mwingine wa kumpenda, ni rahisi kwa mtu kuwa mchoyo—kuwa na wasiwasi na mahitaji yao, matakwa, na maslahi yao. Kama mtu binafsi hauitaji kumfikiria mtu mwingine ambaye ni muhimu unapotaka kusafiri kwa ghafla, kuchelewa kurudi, au kuchukua kazi mpya.

Ongeza mtu mwingine kwenye picha hiyo, na sasa, unapaswa kumfikiria mtu mwingine. Unatoa na kupokea upendo. Lakini katika hali hii, bado inaweza kuwa rahisi kutoka kwenye upendo safi na kuwa mchoyo wakati mnapojikita katika kutarajia mahitaji yenu yatimizwe na mwingine.

Lakini upendo kamili usio na ubinafsi kamwe na daima unaowajenga wengine ndio unatoka kwa Mungu.

Tunaweza kuona hili katika Utatu wa Mungu.

Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu wako katika mwendo wa kudumu wa kutumikiana na kutoa upendo kwetu. Agano la Kale linaonyesha upendo huu wa Mungu, ikitumia neno hesed, ambalo ni sawia na la Kigiriki agape.

Hesed ina kina kisichoweza kueleweka. Gibson anajadili hili katika kitabu chake A God Named Desire:

“Kama manabii wa Kiebrania walivyofanya juhudi za kumfafanua Mungu na kumfikia, hesed ndio neno waliolitumia mara nyingi zaidi kuliko lingine lolote, mara nyingi wakiliunganisha na maneno mengine kujaribu kupanua maana yake tajiri.”6

Hesed inatafsiriwa kama rehema, wema, fadhili, na wema wa milele—kutaja mifano michache ya Kibiblia.7

Inabeba mawazo ya:

  • Utiifu
  • Uadilifu
  • Uaminifu
  • Uthabiti
  • Kujitoa

Huu ndio upendo ambao Mungu anao kwa kila mmoja wetu. Ni upendo wa kina sana kiasi cha kutovunja ahadi yake kwetu badala yake alikuja akafa kwa ajili yetu – hata kama hatuchagui kupokea zawadi hiyo:

“Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi” (Warumi 5:8, UV030).

Kama aya hii inavyosisitiza, upendo huo pia ni upendo usio na masharti. Mtaalam wa theolojia John Peckham, PhD, ambaye ameandika vitabu kuhusu upendo wa Mungu, anasema:

“Upendo wa Mungu daima ni upendo ambao hatustahili. Haupatikani kwa juhudi. Sio kitu ambacho lazima ulipie ili upokee.”8

Na Mungu aliamua kutupenda kwa namna hii, bila kujali kama tutampenda pia. Anatupa uhuru kamili wa kuingia katika uhusiano naye au la kwa sababu anajua kwamba upendo wa kweli hauwezi kulazimishwa.

Lakini je, Mungu anatupenda kwa sababu ya kanuni tu—kwa sababu anaona ni jambo sahihi na anachagua kufanya hivyo? Au anatufurahia na anatuhitaji?

Picha inaendelea kuwa bora zaidi.

Agape au phileo?

Ikiwa tutaishia kwenye agape, tunakosa upande muhimu wa upendo wa Mungu. Aya katika Agano Jipya pia hutumia phileo kuueleza.

Angalia mfano huu wakati Yesu alipokuwa akizungumza na wanafunzi wake:

“kwa maana Baba mwenyewe awapenda [phileo]” (Yohana 16:27, UV030).

Na mtume Paulo anatumia neno phileo kueleza upendo tunapaswa kuwa nao kwa Mungu (1 Wakorintho 16:22).

Yaani, upendo wa Mungu sio wa kanuni tu, wa kujitoa kafara. Pia anaelekeza upendo na hisia kwetu. Agape na phileo zote zinaonyesha upendo wake.

Peckham anakubaliana:

“Tumezoea kufundishwa kwamba agape ndio neno pekee linaloeleza upendo wa Mungu, na ni aina bora ya upendo, na aina zingine zote za upendo ni duni. Lakini katika Yohana 16:27, Mungu anaeleza upendo wake Mwenyewe kama phileo.”9

Agape na phileo zinafanya kazi pamoja, kama mwandishi mwingine wa Kiadventista anavyo andika:

“Aina zote za upendo zinafanya kazi kwa ukamilifu na zote ni njia halisi ya kueleza upendo; zote zikiwa sehemu ya uumbaji wa Mungu. Aina zote za upendo zinaweza kufanya kazi katika mahusiano ya binadamu kwa binadamu, Mungu kwa binadamu, na binadamu kwa Mungu.”10

Kadri tunavyojifunza kuhusu upendo wa Mungu, bado kuna maswali fulani yanayobakia, hata hivyo, kuhusu hasira na haki ya Mungu. Mambo hayo yanakaaje katika picha moja?

Upendo wa Mungu dhidi ya haki Yake?

A scale and gavel, both symbols of justice

Photo by Sora Shimazaki

Ikiwa Mungu ni upendo, basi kila kitu ambacho ni kweli juu yake lazima kiwe kweli kwa sababu yeye ni upendo. Yeye ni mwenye huruma kwa sababu yeye ni upendo. Yeye ni mwenye fadhili kwa sababu yeye ni upendo. Na yeye pia ni mwenye haki kwa sababu yeye ni upendo.11

Kama Peckham anavyosema, “Upendo na haki ya Mungu vinakwenda pamoja. Kwa sababu ukimpenda mtu, utaumizwa na dhuluma zozote zinazofanywa dhidi yake.”12

Fikiria jinsi unavyoweza kuhisi ikiwa mtu angemteka mtoto wako na kumdhuru kwa njia fulani. Ungekasirika na kuwa tayari kupata haki.

Na je, Mungu anataka haki kiasi gani zaidi kwa watoto wake ambao wameonewa? Mtaalam wa theolojia wa Waadventista Angel Rodriguez, ThD, anaonyesha wazi:

“Upendo na ruhusa haviwezi kulingana…. Upendo wa Mungu ni upendo mgumu.”

Tunaweza kupata faraja katika hilo kwa sababu inamaanisha Mungu ataleta haki kwa niaba yetu.

Lakini hii inaweza kuonekana kama mada ngumu. Unaweza kujiuliza kwa nini hujaona haki ikitolewa kwa wale waliokuumiza au kukukosea. Kwa nini maisha yaonekane kwenda vizuri kwa mtu fulani ambaye amesababisha maumivu mengi maishani mwako? Wanawezaje kuendelea na maisha licha ya walichofanya?

Hapa ndipo tunaporudi kwenye upande muhimu wa upendo: uhuru.

Mungu amemuumba kila mtu kwenye sayari hii—na wote ni watoto wake. Shauku yake kuu ni kwamba wapate kujua upendo wake na, kama matokeo, waonyeshe upendo huo kwa wengine. Lakini kamwe hatawalazimisha kupokea upendo wake na kuishi kulingana nao, hivyo inamaanisha kwamba watoto wake mara nyingine wanaweza kufanya maamuzi yanayodhuru watoto wake wengine.

Hilo linamweka Mungu katika mkanganyiko, sivyo?

Kwa sababu anathamini uhuru sana, anapaswa kuruhusu uovu ufuate mkondo wake. Vinginevyo, shetani, katika mgogoro huu kati ya mema na mabaya, angekuwa na nafasi ya kumshitaki Mungu kwa kulazimisha upendo wake kwetu.

Jambo jema ni kwamba, hata hivyo, wakati utafika ambapo haki itatendeka—wakati wote watakapokuwa wamepata fursa ya wazi ya kuchagua kuwa upande wa au dhidi ya Mungu. Wakati wa hukumu katika siku za mwisho, Atatambua maamuzi ambayo watu wamefanya na kuleta haki ya mwisho kwa watoto wake wote ambao wameumizwa.

Kwa maelezo zaidi kuhusu haki ya Mungu na swali la uovu,

Yesu anasema nini kuhusu upendo?

Yesu alikuja duniani hapa kutuonyesha Baba na hivyo kutuonyesha tabia yake ya upendo. Maisha yake yalikuwa mfano hai wa upendo wa agape na phileo alipowaponya wagonjwa, kuwagusa wale wenye ukoma, kuwakumbatia waliotengwa na jamii, kuwabariki watoto, na kukemea unafiki wa viongozi wa kidini.

Matendo yake yaliyapa nguvu mafundisho yake kuhusu upendo, ambayo tutayafupisha katika vipengele vitatu:

Mungu Baba anatupenda

Labda maneno yenye nguvu zaidi—na yenye kukumbukwa zaidi—ambayo Yesu aliwahi kusema ni haya:

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele” (Yohana 3:16, UV030).

Ni rahisi kuyaruka maneno haya, kushindwa kuelewa kile yanachomaanisha kwa kweli.

Tazama mfuatano: Mungu alipenda. Kwa hivyo, Akatoa.

Na Yesu alipokuja, alitupenda kwa upendo ule ule wa kujitoa (Yohana 15:9). Alionyesha upendo mkubwa zaidi kwa kujitoa uhai wake kwa ajili yetu (Yohana 15:13). Sasa, anatuita na kutuwezesha kufanya vivyo hivyo.

Upendo ndiyo kitovu cha Amri Kumi

A Bible open to Exodus 20, which contains the Ten Commandments, principles of love for God and love for others

Photo by Tim Wildsmith on Unsplash

Yesu alifundisha kwamba Amri Kumi ni kanuni za kumpenda Mungu na kuwapenda wengine:

“Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” (Mathayo 22:37-40, UV030).

Alihimiza kwamba kutii maagizo haya hakumfanyi mtu kupata wokovu. Badala yake, ni ushahidi wa upendo kwake na kwa wengine:

“Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye” (Yohana 14:21, UV030).

Amri hizi zinakwenda zaidi ya matendo ya nje hadi kwenye moyo wenyewe. Yesu alitaka wafuasi wanaofunua upendo wake zaidi ya wafuasi ambao walifuata taratibu tu (Luka 11:43).

Marko 12 inarekodi maneno yaleyale ya Yesu ambayo tuliyonukuu kutoka Mathayo 22. Baada ya Yesu kueleza jinsi upendo ulivyokuwa muhimu katika Sheria, mtu mmoja katika hadhira yake aliitikia kwa maneno haya:

“na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhahibu zote pia” (Marko 12:33, UV030).

Yesu alimthibitisha:

“Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu” (Marko 12:34, UV030).

Mungu huthamini utii wa kweli, unaosukumwa na upendo, kuliko kufuata tamaduni au sherehe.

Upendo kwa wenzetu ni sehemu ya uanafunzi wetu kwa Yesu

Yesu aliwaita wafuasi wake wote kupenda kama yeye anavyopenda:

“Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi” (Yohana 13:34-35, UV030).

Hii ni sehemu ya mchakato wa uanafunzi— wa kuwa kama Yeye. Na tunapoonyesha upendo kwa wenzetu, tunafunua upendo wa Kristo kwa ulimwengu (Yohana 17:23).

Inasikika vizuri ikiandikwa, lakini aina hii ya upendo sio rahisi. Inahitaji kupenda wale ambao hawatupendi:

“lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?” (Mathayo 5:44-46, UV030).

Unamshughulikiaje rafiki yule aliye kusaliti kwa kusema habari za uongo kukuhusu, au mwenzako kazini anayeonekana kufurahia kukufanya uishi kwa shida? Ni katika hali hizi ambapo upendo wa kimaadili wa agape wa Yesu unakuwa mgumu zaidi kutekelezwa.

Lakini pia katika hali kama hizi tunaweza kumtegemea yeye kutujaza na aina hiyo ya upendo.

Upendo: uchaguzi kwanza, hisia baadaye

Upendo katika hali yake safi, kama tulivyo jifunza, ni tofauti kabisa na hisia zinazobadilika mara kwa mara ambazo mara nyingi tunazifikiria kama upendo. Ni wa kina zaidi ya hayo. Ni aina ya upendo ambao huvumilia changamoto, ambao huchagua kusalia wakati mambo yanapokuwa magumu.

Kama alivyosema Gibson, “Upendo ni kitendo. Ni kanuni ya ahadi na uaminifu na utiifu, liwalo na liwe.”13

Hii haimaanishi kutokuwa na hisia, ingawa. Lakini una msingi muhimu wa kujitolea na kile Gibson anachokiita “Uadilifu wa mahusiano.”

Kwa msingi huo, hisia huzidi kuwa za kina na zenye maana.

Huu ndio upendo ambao Mungu anao kwa kila mmoja wetu. Na upendo ambao anatualika tuwe nao kila mmoja kwa mwenzake

Makala zilizopendekezwa

  1. Moskala, Jiri, “Love – A Decision and a Verb,” Perspective Digest, vol. 8, no. 1. []
  2. Dinsley, John, “A Kiss of Charity: The Debate over Agape,” Ministry. []
  3. Ibid. []
  4. Gibson, Ty, “Life with God, Season 1 – God Is Love,” Adventist Theological Society. YouTube. []
  5. Gibson, Ty, “The Heart of God,” Truth Link Bible Study #2, []
  6. Gibson, Ty, A God Named Desire, p. 90-91. []
  7. Exodus 20:6; 34:6; Psalm 36:10; Isaiah 54:8. []
  8. Peckham, John, “Life with God, Season 1 – God Is Love,” Adventist Theological Society, YouTube. []
  9.  Ibid. []
  10. Dinsley, “A Kiss of Charity: The Debate over Agape.” []
  11. Gibson, “Life with God, Season 1 – God Is Love.” []
  12. Peckham, “Life with God, Season 1 – God Is Love.” []
  13. Gibson, “Life with God, Season 1 – God Is Love.” []

Je, Una swali kuhusu Waadventista? Uliza hapa!

Pata majibu kwa maswali yako kuhusu Waadventista Wasabato

Majibu Zaidi

Je, Ni Kawaida Wakristo Kuwa na Mashaka?

Je, Ni Kawaida Wakristo Kuwa na Mashaka?

Ndio, ni kawaida kabisa kwa Wakristo kupitia vipindi vya mashaka katika maisha yao ya kiroho. Kila mtu ameshawahi kuwa na mashaka wakati mmoja au mwingine, hata wachungaji, wanatheolojia, na watu muhimu katika Biblia.

Kile Mfano wa Yesu Kinatufundisha Kuhusu Maombi na Kufunga

Kile Mfano wa Yesu Kinatufundisha Kuhusu Maombi na Kufunga

Kufunga na kuomba vilikuwa sehemu muhimu ya huduma ya Yesu Duniani. Hebu tujifunze jinsi mfano wa Yesu unavyoweza kutufundisha jinsi ya kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na Mungu. Kufunga na kuomba vilichukua sehemu kubwa ya huduma ya Yesu Duniani.