Vidokezo 8 vya Ushauri kwa Familia kutoka kwa Ellen White

Familia—inaweza kuwa chanzo cha sehemu yenye kufurahisha na yenye kuleta changamoto katika maisha. Ni katika familia ambapo watu binafsi wanajenga utambulisho wao na kujifunza tabia ambazo zinaweza kuwasukuma mbele au kuwakwamisha katika maisha.

Ellen G. White, mtu muhimu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato, aliamini kwamba ilikuwa muhimu kuandika kuhusu familia kwa sababu ndio msingi wa kanisa na jamii na wanapaswa kuonyesha jinsi Mungu alivyo.

Mara nyingi, hata hivyo, watu wenye shida zaidi za kuelewana nao ni wale tunaowapenda zaidi. Baada ya yote, hao ndio watu wanajua haswa ni vitu gani vya kufanya ili kutukera zaidi.

Lakini licha ya changamoto, familia inaweza kuwa na athari nzuri wakati Yesu Kristo ndiye msingi wetu. Tunapomgeukia kwa hekima, Yeye hutufundisha kuishi kwa neema kati yetu —na pia kujipatia neema.

Katika makala haya, tutachunguza ufahamu ambao Ellen White alipokea kutoka kwa Mungu. Tutajadili mada 8 kuu ambazo alizisisitiza kwa familia:

Tuanze.

1. Weka Mungu kuwa kitovu cha familia yako

A couple holds an open Bible so they can read the Word of God together.

Photo by Cassidy Rowell on Unsplash

Kanuni muhimu zaidi iliyotiliwa mkazo na Ellen White katika maandishi yake yote ilikuwa imani kwa Mungu. Aliandika:

“Dini nyumbani – ni nini isichoweza kukifanikisha? Itafanya kazi ile ile ambayo Mungu alipanga ifanyike katika kila familia. Watoto watalelewa katika malezi na maonyo ya Bwana.”1

Hiyo ni kwa sababu imani na uaminifu kwa Mungu ndio chemchemi ya kila kitu kingine kizuri na cha kupendeza katika maisha yetu. Kupitia Yeye, tunapokea tabia za Roho ambazo ni muhimu katika maisha: upendo, furaha, amani, uvumilivu, upole, wema, uaminifu, upole, na kujidhibiti (Wagalatia 5:22–23).

Imani kwa Mungu, kwa njia ya matendo, inaweza kuonekana kama:

  • Kutenga muda kwa ajili ya maombi binafsi na kusoma Biblia kila siku
  • Kusali pamoja kama familia kuhusu maamuzi makubwa
  • Kujadili kifungu cha Biblia wakati wa chakula
  • Kushiriki katika shughuli za kanisa
  • Kuonyesha neema katika mwingiliano wako na wanafamilia wako

Na kwa kuiga tabia hizi, ni jambo la kawaida zaidi kwamba wale wanaokuzunguka, ikiwa ni pamoja na watoto, watakuwa na hamu ya kuwa na tabia kama hizo katika maisha yao wenyewe.

Vipi kuhusu familia yenye wanafamilia wasioamini?

Labda una mwana familia au mwenzi ambaye imani yake ni tofauti na yako au sio Mkristo. Je, nini kifanyike?

Ellen White, katika visa nyingi, aliona kuwa kulikuwa na tabia kwa wale ambao wenzi wao hawakuunga mkono imani zao kuwa mbali kihisia au hata kufikiria kuondoka katika ndoa. Mwishowe, ilionekana kwamba mitazamo yao kuhusu jinsi ya kuishi maisha na malezi ya watoto ilikuwa tofauti sana!

Hata hivyo, Ellen White alisisitiza kwamba kukatisha ndoa sio suluhisho. Wala haikuwa ni tabia ya kutojali.

Badala yake, alishauri wenzi wa Kikristo kuweka mfano thabiti, wenye subira, na upendo kupitia mambo ya kawaida kama vile:2

  • Kuonyesha tabia ya kujali na kusaidiana, ukibashiri mahitaji yao (bila kukiuka imani au mahitaji yako)
  • Kuwa na subira na uzingatiaji
  • Jikite (na utambue) katika sifa njema za mwenzi wako, sio tu tofauti na changamoto
  • Kuepuka kuhukumu, ukosoaji, au shinikizo la “kuongoka”

2. Dumisha mduara mtakatifu wa faragha

Ellen White alifundisha dhana ya “mduara takatifu” unao zunguka familia.

Kwa kauli hii, alikuwa akimaanisha hisia ya faragha ambayo inapaswa kuhifadhiwa katika familia ili kulinda mioyo ya kila mmoja. Inajenga usalama na imani kwa sababu wanafamilia wanajua kile wanachoshirikiana, ikiwa ni pamoja na makosa yao, haitashirikishwa na wengine.3

Hii haimaanishi kwamba familia isipaswe kamwe kutafuta msaada wa nje, kama vile wa mshauri. Pia haimaanishi kukaa kimya kuhusu unyanyasaji.

Lakini imaanisha kuwa mwangalifu jinsi mambo ya familia yanavyoshughulikiwa.

Hakuna faida katika kufichua mambo machafu. Isipokuwa katika kesi kali kama zile zilizoorodheshwa hapo juu, hakuna mtu nje ya mduara wa familia anahitaji kujua kila maelezo kuhusu matatizo yao, ugomvi kati ya ndugu au mzozo wa ndoa. Ni bora ikiwa mambo hayo yanashughulikiwa ndani ya kuta za nyumba, ikiwezekana. Haihitaji kuwa biashara ya mtu mwingine.

Kupenda wanafamilia wetu kunamaanisha kulinda hisia zao na heshima yao.

3. Tafuta umoja

Umoja sio kutokuwepo kwa tofauti za maoni. Ni kuwa na azimio la kuwa pamoja licha ya tofauti hizo. Ingawa tofauti ni lazima, jambo la muhimu ni kwamba tunafanya juhudi kuelekea suluhisho, huruma, na kuelewana.

Lakini ni rahisi kujikuta mkigombana kuhusu tofauti ndogo na kuzifanya kuwa kubwa. Asili yetu ya ubinafsi inatufanya kutaka kuthibitisha tuko sawa.

An Adventist family holding hands as they pray over a meal

Photo by Tima Miroshnichenko

Katika kushauri familia, Ellen White aliwaonya kuhusu hili:

“Wazazi wanapaswa kuwa makini wasiruhusu roho ya ugomvi kuingia nyumbani; kwa sababu hii ni moja ya mawakala wa Shetani kuacha alama yake kwenye tabia. Ikiwa wazazi watapambana kwa umoja nyumbani kwa kufundisha kanuni zilizo tawala maisha ya Kristo, ugomvi utatoweka, na umoja na upendo utadumu hapo.”4

Watoto ni wepesi kuona kutofautiana kwa wazazi wao, hivyo aliwahimiza wazazi kuweka mfano wa umoja.

Hii inaweza kuonekana kama kuweka kando mjadala ambao haionekani kuendelea na kurudi baada ya maombi. Na inaweza kuhusisha kuacha kando mapendeleo binafsi ili kufikia hatua ya makubaliano na mpango ulio unganishwa.

Lakini mwishowe, umoja huu unaanza na wenzi wote wakikaribia zaidi kwa Kristo na kanuni zake katika Neno lake.

Ellen White alitumia mfano wa nzirani kwenye gurudumu. Kadiri nzirani zinavyokaribia katikati ya gurudumu, ndivyo zinavyokaribiana.5 Vivyo hivyo, kadiri wanafamilia wanavyomkaribia Kristo, ndivyo wanavyokuwa pamoja zaidi.

Kujenga umoja katika familia yako, kwanza tafuta binafsi kumkaribia Kristo kupitia kusoma Biblia na sala. Unapofanya hivyo, unaweza Kumwona akionyesha maeneo katika maisha yako ambapo unahitaji kuachilia mapendeleo yako ili kutafuta mambo yaliyo bora kwa wale wanaokuzunguka.

Lakini tunapaswa kuzingatia kwamba umoja unaotokana na Kristo sio ufanano. Zaidi kuhusu hilo tutalizungumzia baadaye.

4. Saidia kila mtu kuwa na utu wao.

Upendo na heshima ni tabia muhimu katika nyumba inayostawi, lakini haiwezi kutokea bila kanuni ya uhuru wa uchaguzi na utu binafsi.

Kwa sababu hiyo, Ellen White alikumbusha watu mara kwa mara kwamba “hakuna mtu anapaswa kukubali kuwa mashine, inayoongozwa na akili ya mtu mwingine. … Simama katika utu wako uliopewa na Mungu. Usiwe kivuli cha mtu mwingine.”6

Alipokuwa akitoa ushauri kwa mwanamke ambaye alikuwa akifikiria ndoa, Ellen White alimhimiza mwanamke kuuliza ikiwa “atakuwa na ruhusa ya kudumisha utu wake, au lazima maamuzi yake na dhamiri yake zisalimishwe chini ya udhibiti wa mumewe?”7

Wakati mipaka hii inavukwa na mazingira ya nyumbani yanakuwa yenye sumu, jitoe katika hali hiyo na usisite kuomba msaada kwa ajili yako na kulinda watoto wako.8

5. Tanguliza maendeleo ya tabia

A father instructing his daughter on how to wash her hands

Photo by CDC on Unsplash

Nyumbani ndio shule ya kwanza ya watoto na mahali ambapo wanajifunza tabia muhimu ambazo watazibeba maishani mwao. Kadiri uwezavyo, fanya hili kuwa kipaumbele chako nyumbani – kuliko kuendesha biashara, kuwa na mafanikio kifedha, au hata kuweka nyumba yako safi.9

Ellen White aliwahimiza wazazi “kujiepusha na kila kitu kingine maishani mwao ambacho kinazuia kazi hii [kuwalea watoto] ifanyike, na kuwalea watoto wako kwa mfumo Wake.”10

Kupitia shughuli za kila siku kama kufanya kazi za nyumbani, mahusiano na ndugu, na michezo, tafuta fursa za kuwaelimisha watoto wako katika kanuni kama zilivyotajwa katika kitabu cha Ellen White, Mwongozo wa Malezi ya Watoto:11

  • “Ongoza watoto wako kuwa washindi. Wafundishe kumtazamia Mungu kwa kupata nguvu.”
  • “Waambie kwamba Anasikia maombi yao.”
  • “Wafundishe kushinda uovu kwa wema.”
  • “Wafundishe kutumia ushawishi unaoinua na kuenzi.”
  • “Waongoze kuunganika na Mungu.”

Hata unapowafundisha watoto wako, tafuta njia za kujenga ukaribu nao kwa makusudi. Unaweza kula chakula kimoja pamoja kama familia kila siku, kusoma pamoja kabla ya kulala, au kutenga muda usioingiliwa kucheza nao.

6. Gawanya majukumu

Ellen White aliona familia kama timu inayoshirikiana katika majukumu ya nyumbani badala ya kuyaweka yote kwa mtu mmoja.

Alieleza hivi:

“Kila mwana familia anapaswa kuelewa kuwa ni jukumu lake binafsi kufanya sehemu yake katika kuongeza faraja, utaratibu, na usawa wa familia…. Kila mwanafamilia anapaswa kuelewa sehemu yake anayotarajiwa kuchukua kwa umoja na wengine. Wote, kutoka kwa mtoto mwenye umri wa miaka sita na zaidi, wanapaswa kuelewa kuwa wanatakiwa kubeba sehemu yao ya mizigo ya maisha.”12

Anza watoto wako wakiwa wadogo kwa kuwapa majukumu yanayolingana na umri wao. Kwa mfano, mtoto wa miaka sita hatakuwa tayari kukata nyasi au kupika chakula kamili lakini labda anaweza kukunja taulo au kuambatanisha soksi.

7. Punguza mambo yanayosababisha msongo wa familia

Msongo unaweza kutokea katika njia nyingi—msongo wa kazi, majukumu ya kanisa, shughuli za baada ya shule, na zaidi. Ndio maana Ellen White aliandika:

“Matatizo yanaweza kuvamia, lakini haya ni sehemu ya ubinadamu. Acha subira, shukrani, na upendo uchangamshe moyo ingawa siku inaweza kuwa na changamoto nyingi.”13

Wekeza mipaka ili kuzuia msongo wa kazi au majukumu mengine yasiingie kwenye familia.

Inaweza kuwa mipaka ya muda—kuchagua kutokupokea simu au kujibu barua pepe za kazi baada ya saa 12 jioni au wakati wa mlo wa familia.

Huenda ikawa mipaka ya kihisia— kuwa na matumaini na kutafuta njia za kupunguza msongo, kama vile kucheza na watoto, kwenda kutembea, au kuenda ziara.

8. Unda mazingira ya amani nyumbani.

Two sisters washing and drying the dishes, which helps keeps the house clean and neat

Photo by cottonbro studio

Kwa kuzingatia tabia na mambo ya kiroho, tunaweza kufikiri kwamba mazingira yetu ya nje hayana maana. Lakini Ellen White aliona tabia na mazingira kama muhimu. Alisema:

“Tunapaswa kujihadhari na mapambo na maonyesho yasiyo ya lazima, lakini hatupaswi kuwa watu wasiojali kuhusu muonekano wa nje. Kila kitu kuhusu sisi wenyewe na nyumbani mwetu lazima kiwe safi na kuvutia.”14

Kuwa na nyumba safi na yenye utaratibu kunaweza kusaidia kuunda mazingira ya amani—mahali ambapo wanafamilia watakuwa na hamu ya kutumia muda pamoja.

Ili kukuza mazingira haya, pata njia za kuhusisha kila mtu.

Kwa mfano, wanafamilia wote wanaweza kuwajibika kwa kudumisha usafi wa vyumba vyao na kuchangia katika kudumisha utaratibu wa nyumba nzima. Watoto wanaweza kusaidia kufagia, kuosha vyombo, kutupa takataka, na zaidi. Fanya usafi wa kila msimu, kama vile kufagia majani, kusafisha gereji, au kufuta makabati, kuwa fursa kwa familia kufanya kazi pamoja.

Anza na mabadiliko madogo katika familia yako

Huenda ukajisikia kama huna familia “kamilifu” – kwamba hakuna njia utakayoweza kuifanya timilifu.

Lakini hivyo sivyo Mungu anavyofanya kazi. Anatuita tuweke lengo la kiwango bora, lakini ametupa kanuni tunazoweza kutumia bila kujali hali tunazoweza kukutana nazo.

Basi chukua hatua moja kwa wakati, ukijumuisha mabadiliko madogo. Mungu ameahidi kukupa neema Yake na kukuelekeza njiani.

Kweli, tumegusia kwa kifupi linapokuja swala la ushauri wa Ellen White. Ili kuona zaidi ya aliyosema kuhusu familia, angalia kitabu chake Nyumba ya Mwadventista.

Na ikiwa unajiuliza jinsi ya kuboresha ndoa yako – sehemu muhimu ya familia – pata kanuni za msingi kwenye ukurasa wetu kuhusu mwongozo wa Ellen White kwa ndoa.

Chagua Masomo ya Biblia Mtandaoni

Unataka kuendelea kujifunza? Pata habari zaidi kuhusu Yesu, mwanadamu, mpango wa wokovu, na jinsi Mungu anavyokupenda kiasi cha kutosha kujitolea kila kitu, ili tu kukupatia nafasi ya kumchagua.

Wakati mwingine inaweza kuwa ngumu kujua pa kuanzia, ndio maana tunatoa chaguo za masomo ya Biblia mtandaoni bure, rahisi kutumia, unaweza kufanya wakati wowote, mahali popote, na kwa kasi yako mwenyewe.

Shule hii ya Biblia mtandaoni itakuelekeza kupitia mada kuu za Maandiko, ikivunja dhana ngumu za Biblia katika vipande vidogo, ambavyo vinaweza kukusaidia kupata majibu ya maswali magumu zaidi ya maisha.

Viungo vinavyohusiana

  1. White, Ellen, The Adventist Home, p. 322. []
  2. Ibid., p. 349. []
  3. Ibid., p. 177. []
  4. White, Ellen, “Manuscript 53,” 1912. []
  5. White, Ellen, Letter 49, 1904. []
  6. White, The Ministry of Healing, p. 498. []
  7. White, Ellen, Testimonies for the Church, vol. 5, p. 362. []
  8. White, The Adventist Home, p. 348. []
  9. White, Ellen, Child Guidance, Section 8, pp. 161–190. []
  10. White, The Adventist Home, p. 324. []
  11. White, Child Guidance, p. 172. []
  12. White, Testimonies for the Church, vol. 2, p. 699. []
  13. White, Ellen, The Ministry of Healing, p. 393. []
  14. White, The Adventist Home, p. 22. []

Je, Una swali kuhusu Waadventista? Uliza hapa!

Pata majibu kwa maswali yako kuhusu Waadventista Wasabato

Majibu Zaidi

Ellen G. White Alitoa Ushauri Gani kuhusu muziki?

Ellen G. White Alitoa Ushauri Gani kuhusu muziki?

Ellen G. White Alitoa Ushauri Gani kuhusu muziki?Katika kiini chake, muziki ni mkusanyiko wa sauti, muinuko wa sauti na mapigo ambayo huleta wimbo. Pia ni zaidi ya hayo. Kama aina yoyote ya sanaa, inaweza kuwa nzuri sana au mbaya sana, yenye kusisimua au yenye...

Kuelewa Maisha na Huduma ya Ellen G. White

Kuelewa Maisha na Huduma ya Ellen G. White

Jifunze Ellen G. White ni nani hasa na jukumu alilokuwa nalo katika kuongoza Kanisa la Waadventista Wa Sabato mapema kupitia huduma yake na maandishi yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu.

Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen White

Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen White

Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen WhiteSabato ni mada muhimu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato. Sio jambo la kushangaza, basi, kwamba Ellen G. White, mwanzilishi mwenza wa kanisa, alisoma mafundisho ya Biblia kuhusu Sabato na akaandika kiasi kikubwa...

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. White

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. White

Urithi wa Kudumu wa Ellen G. WhiteEllen G. White ni jina linalojulikana sana miongoni mwa Waadventista wa Sabato, lakini pia aliathiri sehemu nyingi za historia, mbali na kuwa mwanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Ndiyo maana Jarida la Smithsonian...

Wafahamu Watoto wa Ellen White

Wafahamu Watoto wa Ellen White

Ellen White, ambaye ni mmoja wa waanzilishi maarufu zaidi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, alikuwa na watoto wanne na mumewe, James: Henry Nichols, James Edson, William Clarence, na John Herbert.

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa Waadventista

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa Waadventista

Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa WaadventistaWaadventista wa Sabato wanajulikana kwa kusisitiza maisha yenye afya bora. Na Ellen G. White alikuwa na ushawishi mkubwa katika maendeleo ya kipaumbele hiki na utekelezaji wake miongoni mwa Waadventista....