Akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, Ellen G. White alipewa jumbe nyingi, ushauri, ufunuo, na maono kuhusu Biblia, historia, unabii, na jinsi tunavyoweza kutumia kanuni za kibiblia katika maisha yetu ya kila siku.
Alikuwa pia mwanzilishi mwenza anayeheshimika sana wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Basi ni ipi kati ya jumbe hizi kutoka kwa Mungu zilihusiana moja kwa moja na kukuza dhehebu hili?
Mwanzoni mwa Harakati ya Waadventista, walikumbana na maswali mengi kuhusu njia bora za kueneza injili. Walichunguza Maandiko lakini walipambana na mbinu. Wangewezaje kutumia rasilimali zao chache vyema ili kushiriki tumaini la kweli walizogundua katika Biblia?
Na walipokuwa wakiomba mwongozo, Mungu alifanya kile ambacho amekuwa akifanya tangu Agano la Kale ili kuwasaidia watu Wake kuelewa mapenzi Yake vizuri zaidi—kutuma mjumbe (Matendo 26:16-18).
Basi hebu tuangalie maono na mwanga mbalimbali ambao Ellen White alipewa kuhusu maendeleo na uendelezaji wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Ushauri huu ulihusu:
- Kusisitiza kazi ya utume duniani kote
- Kujiunda kama dhehebu rasmi
- Huduma ya uchapishaji
- Maisha yenye afya na kazi ya utume ya tiba
- Elimu
- Kanisa katika siku za mwisho
Na pia tutaangalia jinsi ushauri huu unaoongozwa na Roho bado ni muhimu leo. Lakini hebu tuanze kwa kuangalia jinsi Ellen White alivyolisaidia Kanisa la Waadventista wa Sabato kulingana na agizo kuu la kueneza injili duniani kote.
Kusisitiza kazi ya utume duniani kote

Courtesy of the Ellen G. White Estate, Inc.
Mwanzoni, Kanisa la Waadventista wa Sabato lililenga kushiriki Neno la Mungu na miji na vijiji vya karibu. Lakini mwaka 1874, Ellen White alipata maono—malaika alimwambia kwamba kanisa lazima lifikie ulimwengu mzima.1 Malaika alirejelea Mathayo 5:14-16, akisema, “Nuru yenu isitiwe chini ya pishi wala chini ya kitanda, bali iwekwe juu ya kinara, ili iwaangazie wote waliomo nyumbani. Nyumba yenu ni dunia.”2
Kwa hiyo, Ellen White alileta ujumbe huu kwa viongozi wengine wa kanisa. Juhudi zilianza mara moja za kuwatuma wamishonari katika maeneo ya mbali.3
Msisitizo huu juu ya kazi ya utume ng’ambo unarejelea maneno ya Yesu Mwenyewe, alipowaita wafuasi Wake kueneza neno kwa kila mtu wanayekutana naye, popote waendapo:
“Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari” (Mathayo 28:19-20, UV030).
Kwa kuwa wameuchukua msisitizo huu kwa moyo, programu za utume zimekuwa uwanja mkubwa wa kazi ndani ya kanisa. Hadi sasa, Kanisa la Waadventista wa Sabato lina zaidi ya washiriki milioni 18 duniani kote.4
Waadventista wanaamini kwamba mara injili itakapowafikia wote, Yesu atarudi tena. Na hakuna kitu tunachokisubiri kwa hamu zaidi ya kurudi kwa Mwokozi wetu mara ya pili.
Kuunda Kanisa la Waadventista wa Sabato

Courtesy of the Ellen G. White Estate, Inc.
Kadiri Harakati ya Waadventista ilivyokuwa ikikua, Ellen White hatimaye alipokea maono yaliyofafanua jinsi ingeweza kuwa imara zaidi kwa kuwa taasisi rasmi.5
Wakati huo kanisa halikuwa na jina rasmi,6 na wahubiri wao wengi hawakuwa na vyeti vya kufundisha kwa sababu hakukuwa na mpangilio rasmi.7 Hii ilisababisha ugumu katika kudumisha haki zao za kumiliki mali za kanisa.8
Hapo mwanzo, waumini wengi walikuwa na wasiwasi kuunda kanisa lililoandaliwa.9 Waliogopa kwamba ingezuia juhudi za kimishonari.10
Ingawa wasiwasi wao ulikuwa na msingi, alitambua kile kilicho hitajika ili kutimiza mipango yao. Kisha akawarudisha kwenye Biblia, akieleza kwamba kanisa la kwanza la Kikristo katika Agano Jipya pia lilikuwa limepangwa.11
Maono yake yalizungumzia yafuatayo:12
- Kwamba wanapaswa kuwa na utaratibu na mpangilio huku wakiepuka urasmi usio wa lazima. Inapaswa kuakisi utaratibu wa mbinguni, na wa kanisa la kwanza.
- Kwamba kuwa mwili mmoja ulioungana kungewalinda dhidi ya mashambulizi ya Shetani ya kudhoofisha misheni yao ya kueneza injili.
- Kwamba utaratibu ungewalinda dhidi ya kutegemea wahudumu wasiofaa au wasio na mafunzo.
Na hivyo, baada ya majadiliano mengi, chombo kikuu cha uongozi wa kanisa—Konferensi Kuu—kiliundwa.
Kuwa na shirika rasmi na jina kuliruhusu kanisa kupanua juhudi zake kwa kiasi kikubwa (hasa katika kupanua huduma yake ya uchapishaji).13
Wakati Konferensi Kuu ilipokuwa ikifanya vikao vya mara kwa mara vya kujadili kwa maombi na kupiga kura juu ya maswala muhimu, Ellen White aliishauri kanisa kuhusu sera zaidi, ingawa yeye mwenyewe hakuwahi kushika nafasi ya uongozi wa kiutawala.14 Wakati alitambua kwamba kujiandaa kama kanisa ilikuwa muhimu, bila shaka alitoa ushauri wa tahadhari katika kuendelea.15 Kanisa linapaswa daima kukumbuka mizizi yake.
Makao makuu ya Konferensi Kuu hapo awali yalikuwa Battle Creek, Michigan.16 Na kama kituo cha utawala wa dhehebu, ikawa jamii kubwa ya Waadventista. Lakini kwa kuwa Waadventista wengi waliishi mahali pamoja, alijua walipaswa kuongeza juhudi zao kufikia ulimwengu unaowazunguka. Maono yake yalieleza kwamba wengi zaidi wangeweza kufikiwa kupitia uchapishaji, tiba, na elimu.
Huduma ya uchapishaji

Courtesy of the Ellen G. White Estate, Inc.
Wakati usambazaji wa maandishi ulikuwa ukifanyika tangu mwanzo wa Harakati ya Uadventista, mojawapo ya jitihada kubwa za kwanza kulingana na ujumbe wa Mungu kwa Ellen White ilikuwa kuanzisha jarida rasmi la Waadventista.17 Alimwambia mumewe, James White, kuongoza uanzishwaji wake—ingawa ingegharimu zaidi ya walichoweza kumudu.18
Walijiuliza jinsi gani wangeweza kulipia gazeti hilo. Lakini Mungu alimthibitishia kwamba wasomaji wao wangetoa michango ya fedha.19 Na kweli, walifanya hivyo.
Jarida lao liliongezeka umaarufu na hatimaye likajulikana kama Adventist Review.
Kutoka hapo, idara ya uchapishaji ya Waadventista ilikua na kufikia ulimwengu mzima. Na leo, tuna mashirika 63 ya uchapishaji na vituo 15 vya vyombo vya habari.20 Nyumba kubwa zaidi za uchapishaji zilikuwa Pacific Press, ambayo bado inafanya kazi leo huko Nampa, Idaho, na Review and Herald, ambayo ilifanya kazi hadi 2014.
Hapa kuna muhtasari wa baadhi ya maono yake kuhusu huduma ya uchapishaji ya Kanisa la Waadventista:
- Kuanzisha gazeti la Waadventista: Mwaka 1848, alipata maono yaliyo mwambia atangaze ujumbe wa Kiadventista kwa kutuma chapisho la mara kwa mara. Aliona kwamba lingeanza kwa udogo, lakini lingekua na kuwa jitihada ya kimataifa.21
- Alitiwa moyo kuchapisha gazeti kila wiki: Mwaka 1853, Mungu alimwonyesha kwamba gazeti linapaswa kutoka mara nyingi zaidi. Alipotoa wito wa uhitaji wa uchapishaji wa mara kwa mara, aliwataka Waadventista kutoa na kutumia fedha zao kwa uangalifu zaidi ili wawe na fedha za kuchangia kwenye mambo yanayozihihitaji—kama vile gazeti hilo.22
- Aliambiwa kuwe na nyumba za uchapishaji katika nchi nyingine—hasa Australia: Mwaka 1875 alipata maono kuhusu kueneza nyumba zao za uchapishaji katika nchi nyingine. Aliwasilisha wazo hili kwa kanisa la Battle Creek alipokuwa akijadili njia za kufikia nchi za kigeni na injili.23
Mwisho wa yote, uinjilisti wa vitabu ulisaidia kanisa kukua kwa kutupa nafasi ya kushiriki imani zetu na ulimwengu. Tofauti na uinjilisti wa kawaida, kama mikutano ya hema na mfululizo wa mahubiri, unaweza kuvuka vikwazo vya usafiri na lugha. Vitabu, vijitabu, na majarida vinaweza kusambazwa katika maeneo ambayo Kanisa la Waadventista halikuweza kufika bado, na kutafsiriwa katika lugha mbalimbali.
Na kwa sababu ya ushauri ambao Roho Mtakatifu alitoa kupitia maono ya Ellen White, watu wengi zaidi wamefikiwa na injili.
Maisha yenye afya na kazi ya utume wa kitabibu
Ellen White pia alipokea maono yanayo eleza jinsi kufuata kanuni za maisha yenye afya kunavyotusaidia kuwahudumia wengine vyema, kushiriki injili, na kukuza kanisa.
Katika karne ya 19, wengi walikuwa wagonjwa kutokana na ukosefu wa usafi, lishe bora, na taratibu salama za matibabu. Mungu aliona haja ya kuwaonyesha watu jinsi ya kutunza miili yao ili waweze kuishi maisha marefu na yenye furaha.
Maono haya, ambayo alipewa tarehe 25 Desemba, 1865 huko Rochester, New York, yalimuagiza aanzishe kituo cha afya ili kuwasaidia watu kupona, na kuwafundisha jinsi ya kujitunza vyema.24
Hapa kuna muhtasari wa baadhi ya maono yake kuhusu mada hii:
- Aliambiwa kwamba watu wa Mungu wanapaswa kujihusisha zaidi na matengenezo ya afya: Mwaka 1863, Ellen White alipewa maono yaliyofafanua kwamba kutunza mwili ni wajibu wa kiroho. Hii ni kwa sababu hali ya mwili wa mtu inaweza kuathiri hali yake ya kiakili na kiroho. Ujumbe huu ulikuwa muhimu sana kwa wakati huo kwa sababu Wakristo wengi—wakiwemo Waadventista—walikuwa wakitumia pombe na bidhaa za tumbaku ambazo zilidhoofisha afya yao. Na ingawa tayari alikuwa amepokea maono mwaka 1848 kuhusu hatari za bidhaa hizi, Waadventista wengi bado walikuwa na changamoto ya kuziacha katika maisha yao.
- Aliambiwa ahimize kiasi katika kula: Maono haya yalieleza hatari za kula kupita kiasi.
- Aliambiwa ahimize tabia nzuri za kula na kula kile kilicho “cha kiafya”: Maono haya yalionyesha Ellen White tabia nzuri za kula kama vile kula kwa nyakati maalum, na kuepuka kula kati ya milo. Pia yalionyesha kwamba chakula cha asili cha Edeni—matunda, nafaka, na karanga—ndicho chakula bora kwa mwili wa mwanadamu.
- Aliambiwa waweke sanitariamu za kiadventista vijijini badala ya mijini: Mwaka 1901, akiwa Los Angeles, California, Ellen White alipata maono yaliyo mwambia waweke sanitariamu zao vijijini. Maono hayo pia yaliorodhesha faida za kiafya za mwanga wa jua, hewa safi, na kazi nyepesi za mikono. Alipokea ujumbe huu wakati viongozi wa kanisa walikuwa wakijadili mahali pa kufungua sanitariamu mpya.
Maono hayo yalimuonya kuhusu hatari za pombe, tumbaku, na lishe isiyo na uwiano, hivyo akawapa watu waliomzunguka maarifa hayo.25 Ushauri aliotoa ulikuwa wa kimapinduzi kwa wakati wake, kwani wengi hawakujua madhara ya chaguzi hizi.
Alielekezwa hata katika maono yake mahali pa kuanzisha vituo hivi vya matibabu. Kwa kweli, alisaidia kuchagua maeneo ya sanitariumu za Paradise Valley, Glendale, na Loma Linda.26
Ellen White aliona kwamba vituo hivi vinapaswa kuwasaidia watu kukua kiroho. Kama vile Yesu alivyowahudumia wagonjwa, alielewa kwamba kanisa linaweza kuwafikia watu kwa kuhudumia mahitaji yao ya kimwili.
Tangu wakati huo, mfumo wa huduma za afya wa Kiadventista umekua. Na hadi leo, Kanisa la Waadventista lina takriban hospitali 200.27
Elimu

Courtesy of the Ellen G. White Estate, Inc.
Mfumo wa elimu wakati wa Ellen White haukuwa wa kuridhisha. Watoto wengi walijifunza kuhusu maisha kwa sababu wazazi wao waliwachukua kazini nao kwenye viwanda vya karibu.
Hawakupewa fursa ya kujifunza stadi za msingi kama kusoma au kuandika. Na walikuwa na ufahamu mdogo sana kuhusu Biblia.
Kutokana na athari za Mapinduzi ya Viwanda, malengo mengi ya elimu wakati huo yalikuwa kuwafundisha watoto kwa ajili ya maisha ya kazi viwandani, au kuwafanya wajifunze kazi ile ile wazazi wao waliyoifanya.
Ellen White alijua kwamba kulikuwa na haja ya kufanya jambo kuhusu elimu ya vijana. Alivutiwa na kusaidia watoto wapate utoto bora zaidi huku akikuza ukuaji wa kanisa kupitia elimu ya Kiadventista.
Mungu alimpa mwanga wa kuanzisha shule za kanisa, ambapo wanafunzi wangeweza kukua kielimu na kiroho.28
Hata alimwonyesha maeneo bora kwa ajili ya shule kadhaa za Waadventista.29
Kwa moja ya maeneo haya hasa, hata hivyo, washiriki wengi wa kanisa walikuwa na mashaka kuhusu mahali ilipowekwa Chuo cha Avondale huko Cooranbong, Australia. Walihisi kwamba hapakuwa pazuri kwa ajili ya shamba la shule waliokuwa wamepanga kuliweka hapo.30
Lakini kwa sababu alikuwa anafuata mwongozo wa Roho Mtakatifu, na sio matakwa yake binafsi, Ellen White alisisitiza kwamba ingekuwa mahali bora kabisa—na hata alikuwa anaweka baadhi ya fedha zake mwenyewe ili kununua ardhi hiyo.31
Kisha yote yalikuwa wazi kwamba huu ulikuwa uamuzi sahihi. Kwa sababu watu walidharau ardhi hiyo, kanisa liliweza kuinunua kwa bei ya chini, na hivi karibuni Chuo cha Avondale kikawa taasisi inayostawi.32
Tangu wakati huo, shule nyingi zaidi za Kiadventista zimeanzishwa. Na leo, shule za Kiadventista ndizo mfumo mkubwa zaidi wa shule za Kiprotestanti duniani kote.33
Muhtasari wa baadhi ya maono yake kuhusu mada hii umeorodheshwa hapa:
- Aliambiwa jinsi shule za Kikristo zinavyopaswa kuendeshwa ili kuwafundisha wanafunzi kuwa wafuasi bora wa Kristo: Wakati viongozi wa kanisa walikuwa wakijadili jinsi ya kuendesha shule za Kiadventista, Ellen White alipata maono usiku wa manane yakimwonyesha jinsi shule za Kiadventista zinavyopaswa kuwa. Baadhi ya dhana hizi zilijumuisha kuanzisha shule vijijini ambako wanafunzi wangepata mazingira bora zaidi, na kuwafundisha wanafunzi thamani ya kazi za mikono.
- Aliambiwa anunue eneo la Avondale: Mwaka 1894, Mungu alimwonyesha Ellen White kwamba eneo ambalo kanisa lilichagua na lililoonekana kuwa “kame” lingefaa kabisa kwa ajili ya shule ya Avondale.
- Alionyeshwa mahali kwa ajili ya Chuo Kikuu cha Loma Linda: Baada ya kurudi kutoka Australia, Ellen White alielekezwa kwamba kanisa linapaswa kuanzisha sanitariamu nyingi zaidi kusini mwa California. Alionyeshwa maeneo maalum—moja ikiwa ni eneo ambalo baadaye lingekuwa na Sanitariamu ya Loma Linda ambayo baadaye ilipanuka na kuwa Chuo Kikuu cha Loma Linda.
Mwisho wa yote, ilikuwa ni maono haya yaliyolionyesha kanisa jinsi ya kukua na kushuhudia kwa wengine kupitia huduma yao. Na kwa maendeleo tuliyopata, tukawa kanisa la ulimwengu mzima.
Maono haya hayakutoa tu mwongozo wa kueleza jinsi kanisa linavyoweza kukua—yalitabiri pia jinsi kila huduma hizi zingesambaa na kuwafikia watu duniani kote. Na kwa kumtegemea Roho Mtakatifu, Kanisa la Waadventista likawa shirika kama lilivyo leo.
Ni maono gani Ellen White aliyapata kuhusu kanisa katika siku za mwisho?

Photo by Ben White on Unsplash
Ellen White pia alipata maono mengi kuhusu changamoto zitakazowakabili Wakristo katika siku za mwisho.
“Siku za mwisho” zinarejelea kipindi cha mwisho cha historia ya dunia, kabla tu ya Yesu kurudi katika Kurudi Kwake Mara ya Pili. Katika siku za mwisho, watu wa Mungu wanapewa jukumu la kueneza injili kwa maeneo na watu ambao bado hawajafikiwa (Mathayo 24:14).
Lakini tunapongoja Yesu arudi, matukio mengi muhimu zaidi yatatokea. Ili kuwaandaa watu vyema, Mungu alimpa Ellen White maono yaliyofafanua majaribu ambayo Kanisa la Waadventista lingeyakabili hivi karibuni.
Baadhi ya maono na unabii wake kuhusu nyakati za mwisho ni pamoja na:34
- Hatari za upantheismu: Baadhi ya viongozi na washiriki wa Kanisa la Waadventista walikubali upantheismu na kujaribu kuuleta kanisani. Lakini Ellen White alionyeshwa katika maono aonye dhidi yake. Alikuwa na ndoto ya meli iliyokuwa karibu kugongana na barafu kubwa. Nahodha katika ndoto hii aliwaamuru wafanyakazi wake “kukabiliana nayo” moja kwa moja. Meli iligonga barafu hilo, na barafu likavunjika vipande vipande, lakini meli na wafanyakazi wake walikuwa salama. Alielewa kwamba barafu hilo lilikuwa ni ishara ya ushawishi wa upantheismu. Hivyo alilikabili moja kwa moja kwa kuonya kanisa kuhusu hilo katika mikutano ya hadhara. Kwa ushauri wake wa hekima, kanisa liliamua kulikabili swala hilo na kujadili wazi wazi jinsi linavyopingana na mafundisho ya maandiko.
- Kuibuka kwa roho ya umizimu: Mwaka 1849 alipata maono yaliyomwonya kuhusu kukubalika kwa kasi kwa roho za mizimu, au kujaribu kuwasiliana na wafu. Tayari ilikuwa ni dhana ya kawaida huko Rochester, New York, ambapo watu wangesikia vitu na kuvihusisha na mizimu au roho. Matukio haya yalijulikana kama “kupiga” au “kubisha.” Lakini alitabiri kwamba baadhi ya aina za roho ya umizimu (wakati mwingine huitwa unajimu) zingefundishwa hata katika makanisa ya Kikristo, hivyo Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu na kupima mawazo yote mapya kwa kulinganisha na Biblia.
- Kwamba watu wataweka sayansi dhidi ya dini:35 Nadharia ya mageuzi ya Charles Darwin ilienea wakati wa maisha ya Ellen White. Alionya kwamba watu wengi zaidi wangekubali nadharia hiyo. Lakini Biblia haikukusudiwa kuwa kinyume na sayansi.
Wakati mambo mengi kati ya haya yalikuwa ya tahadhari, maono yake ya mwaka 1857 yalijumuisha pia habari ya matumaini kwamba katika fursa za mwisho kabla ya Yesu kurudi, watu wengi zaidi watakubali injili.36
(Taasisi ya Ellen G. White imekusanya maandiko ya Ellen G. White kuhusu mwisho wa wakati katika kitabu kiitwacho Matukio ya Siku za Mwisho. Pamoja na kitabu chake maarufu, Pambano Kuu, kuna ufahamu mwingi unaotolewa kuhusu kile kitakachotokea katika kipindi cha muda kabla tu ya kuja kwa pili kwa Yesu.)
Ni kweli kwamba mambo mengi ya kutisha yatatokea katika siku za mwisho. Lakini hatupaswi kuyakabili kwa hofu au wasiwasi. Yesu anataka tuwe na ufahamu wa matukio haya ili tuweze kumtumainia kwa mwongozo na ulinzi.
Na ingawa maono ya Ellen White yanaweza kujumuisha marekebisho au maonyo juu ya jambo hili, hatimaye yanalenga kumpa msomaji tumaini katika Yesu. Kwa sababu hata kama tutapitia nyakati ngumu, tunaweza kupumzika katika uhakika kwamba Mungu atatuongoza kupitia yote.
Na jambo la ajabu kuhusu siku za mwisho kutimia ni kwamba hivi karibuni tutamwona Mwokozi wetu uso kwa uso!
Jinsi maono ya Ellen White yalivyo muhimu pia leo

Photo by Brian Erickson on Unsplash
Maono mengi ya Ellen White yalikuwa na athari ya moja kwa moja kwa kanisa—iwe ni kwa kupendekeza mwelekeo wa huduma au kuwaongoza watu kurudi kwenye kweli za Biblia zilizokuwa zimesahaulika.
Na ingawa kuna maono fulani aliyopata ambayo yalikuwa mahsusi kwa wakati wake—kama vile ushauri uliotolewa kwa watu maalum au mwongozo wa jinsi ya kuishi katika karne ya kumi na tisa—sehemu kubwa ya kile alichopokea kupitia kipawa chake cha unabii bado kina umuhimu hadi leo.
Kwa mfano, maono yake kuhusu kuishi kiafya yanatoa taarifa bora juu ya jinsi bora ya kutunza akili na miili yetu. Na kwa kuwa matatizo ya afya yanaongezeka na viwango vya unene kupita kiasi vikipanda, ujumbe huu unaweza kuwa muhimu kuliko wakati mwingine wowote.
Isitoshe, mchango wake katika nyanja za kazi za kimishonari, huduma ya afya, na elimu bado unaathiri watu kote duniani.
Pia anatoa ushauri juu ya jinsi ya kumkaribia Mungu, na jinsi ya kutumia kanuni za Kikristo katika kila sehemu ya maisha. Ingawa tunaweza kukutana na changamoto tofauti leo kuliko watu wa wakati ule, anatukumbusha tuzingatie yale yaliyo ya muhimu kweli. Katikati ya usumbufu na mkanganyiko, anatusihi tuelekeze mawazo yetu kwa Yesu Kristo.
Kwa kweli, kusudi zima la maono ya Ellen White lilikuwa ni kumrejesha Yesu na neno Lake. Hii inaweza kuwa ndiyo sababu “roho ya unabii” inatajwa kama “ushuhuda wa Yesu” katika Ufunuo 19:10.
Ukweli kwamba Mungu anachukua muda kuwavuvia na kuwaongoza manabii unaonyesha jinsi anavyotujali sana. Anataka kutumia karama ya unabii kuondoa mkanganyiko na hofu katika maisha yetu ya kila siku. Anataka kujibu maswali yetu na kutuhakikishia wokovu kupitia kwake.
Watu wa Mungu wanapomwomba mwongozo, Yeye hawaachi gizani. Badala yake, anawapa Roho Wake Mtakatifu na wakati mwingine hutuma wajumbe maalum kuwaonyesha jinsi ya kuishi kama Yesu.
Katika miaka yake mingi ya kumtumikia Bwana, Mungu aliendelea kuongoza mashauri ya Ellen White kwa maono zaidi, ambayo aliyandika na yanaweza kupatikana katika vitabu kama Pambano Kuu, Shuhuda kwa Kanisa, na Jumbe zilizochaguliwa.
Sio vigumu kuona jinsi Ellen White aliweza kuchukua nafasi kubwa katika kuongoza Kanisa la Waadventista kwa uongozi wa Roho Mtakatifu. Kuanzia kuthibitisha mafundisho ya kibiblia kuhusu patakatifu pa mbinguni hadi Hukumu ya Upelelezi hadi kuwaonya waumini wa kwanza wa dhehebu hili kuhusu mitego na vishawishi vya kawaida vinavyohusiana na uendeshaji wa kanisa, Mungu alimtumia kuathiri na kusaidia waumini wenzake katika kueneza injili Yake.
Ikiwa ungependa kujifunza zaidi kuhusu vitabu na makala za Ellen White, angalia,
Au, kama ungependa kujua zaidi kuhusu mafundisho ya Waadventista kwa ujumla,
Tafuta Kanisa
If you’re interested in finding a local Adventist church near you, you can use the Adventist Locator provided by the General Conference of Seventh-day Adventists.
Kurasa Zinazohusiana
- Pfandl, Gerhard, “Ellen G. White’s contributions to the Seventh-day Adventist Church,” https://www.ministrymagazine.org/archive/2015/06/egw [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- “To Every Nation,” https://adventistreview.org/issue-archives/page-2015/page-1515/1515-18/ [↵]
- White, G. Ellen, Early Writings, p. 97. [↵]
- Douglass, E. Herbert, Messenger of the Lord, p.184. [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- Early Writings, p. 97. [↵]
- White, Arthur L., Ellen G. White: Volume 1—The Early Years: 1827-1862, pp. 216, 286-289, 420-424, 437-440, 445-461. [↵]
- Messenger of the Lord, p. 184. [↵]
- Ibid, p.185. [↵]
- Ibid, p. 184. [↵]
- Ibid. [↵]
- Pfandl, https://www.ministrymagazine.org/archive/2015/06/egw [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- “To Every Nation,” https://adventistreview.org/issue-archives/page-2015/page-1515/1515-18/ [↵]
- White, Ellen G., Life Sketches of Ellen G. White, pp. 125-128, 283; White, Arthur L., Ellen G. White: Volume 1—The Early Years: 1827-1862, pp. 163-164. [↵]
- Early Writings, p. 95. [↵]
- Life Sketches, p. 283. [↵]
- Pfandl, https://www.ministrymagazine.org/archive/2015/06/egw [↵]
- Douglass, https://egwwritings.org/read?panels=p656.1678&index=0, p.162. [↵]
- Ibid, p. 163. [↵]
- “Hospitals and Sanitariums,” https://www.adventistdirectory.org/default.aspx [↵]
- Pfandl, https://www.ministrymagazine.org/archive/2015/06/egw [↵]
- Douglass, https://egwwritings.org/read?panels=p656.1898&index=0, p. 190. [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- Ibid. [↵]
- Pfandl, https://www.ministrymagazine.org/archive/2015/06/egw [↵]
- https://ellenwhite.org/correspondence/184345 [↵]
- White, Last Day Events, p. 176. [↵]
- Ibid. [↵]
Majibu Zaidi
Je, Kila Kitu Alichosema Ellen White Kilikuwa na Uvuvio wa Kiungu?
Je, Kila Kitu Alichosema Ellen White Kilikuwa na Uvuvio wa Kiungu?Kanisa la Waadventista Wasabato linaamini kwamba ujumbe mwingi wa Ellen White ulikuwa ufunuo kutoka kwa Mungu. Lakini hiyo haimaanishi kwamba kila kitu alichowahi kusema kilikuwa cha kinabii, au...
Je, Kweli Ellen G. White Alikuwa Nabii?
Ukiangalia yale ambayo Maandiko yanatolewa kama vipimo vya nabii wa kweli, Ellen White anakidhi vigezo vyote.
Mambo Ambayo Ellen G. White Alisema Kuhusu Kutumia Biblia katika Elimu
White, mmoja wa waanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, aliamini kwamba elimu haikuwa kamili isipokuwa ilipojengwa juu ya kanuni za Biblia.
Ushauri wa Kiroho wa Ellen White kuhusu Ndoa
Kama mmoja wa waasisi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato, Ellen G. White aliheshimiwa sana.
Mafundisho ya Ellen G. White kuhusu Elimu ya Chuo
Ellen G. (Harmon) White, mwanzilishi muhimu wa Waadventista wa Sabato, mara nyingi anajulikana kwa mwongozo wake wa vitendo na kiroho kuhusu elimu sahihi kwa watoto.
Maono na Unabii wa Ellen White
Agano Jipya linathibitisha unabii kama karama ya Roho ambayo itaendelea hadi mwisho wa wakati (Waefeso 4:11–14).
Vidokezo 8 vya Ushauri kwa Familia kutoka kwa Ellen White
Familia—inaweza kuwa chanzo cha sehemu yenye kufurahisha na yenye kuleta changamoto katika maisha.
Ellen G. White Alitoa Ushauri Gani kuhusu muziki?
Ellen G. White Alitoa Ushauri Gani kuhusu muziki?Katika kiini chake, muziki ni mkusanyiko wa sauti, muinuko wa sauti na mapigo ambayo huleta wimbo. Pia ni zaidi ya hayo. Kama aina yoyote ya sanaa, inaweza kuwa nzuri sana au mbaya sana, yenye kusisimua au yenye...
Mwongozo wa Ellen G. White kuhusu Elimu ya Kikristo
Ellen White, mwanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, aliona kuwa mfumo wa elimu nchini Marekani wakati wake ulikuwa haukidhi mahitaji.
Hazina ya Ellen G. White Ni nini ?
Mchango wa Ellen G. White katika uundaji na ukuaji wa Kanisa la Waadventista wa Sabato ni sehemu muhimu ya historia yake.
Kuelewa Maisha na Huduma ya Ellen G. White
Jifunze Ellen G. White ni nani hasa na jukumu alilokuwa nalo katika kuongoza Kanisa la Waadventista Wa Sabato mapema kupitia huduma yake na maandishi yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu.
Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen White
Sabato katika Maisha na Mafundisho ya Ellen WhiteSabato ni mada muhimu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato. Sio jambo la kushangaza, basi, kwamba Ellen G. White, mwanzilishi mwenza wa kanisa, alisoma mafundisho ya Biblia kuhusu Sabato na akaandika kiasi kikubwa...
Urithi wa Kudumu wa Ellen G. White
Urithi wa Kudumu wa Ellen G. WhiteEllen G. White ni jina linalojulikana sana miongoni mwa Waadventista wa Sabato, lakini pia aliathiri sehemu nyingi za historia, mbali na kuwa mwanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Ndiyo maana Jarida la Smithsonian...
Hatua Kuelekea kwa Kristo: Mwongozo wa Uhusiano na Yesu
Iwe unanza safari yako na Yesu Kristo, unarejea baada ya muda fulani, au umekuwa na uhusiano na Yesu kwa miaka, kutumia kitabu
Wafahamu Watoto wa Ellen White
Ellen White, ambaye ni mmoja wa waanzilishi maarufu zaidi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato, alikuwa na watoto wanne na mumewe, James: Henry Nichols, James Edson, William Clarence, na John Herbert.
Jinsi Mafundisho ya Ellen White Yanavyoweza Kuboresha Afya Yako
Matibabu katika karne ya kumi na tisa yalisemekana kuacha “ugonjwa zaidi kuliko yalivyotibu” kwa matumizi yake ya kutoa damu na “dawa” kama zebaki na arseniki.
Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa Waadventista
Jinsi Ellen White Alivyochangia Ujumbe wa Afya wa WaadventistaWaadventista wa Sabato wanajulikana kwa kusisitiza maisha yenye afya bora. Na Ellen G. White alikuwa na ushawishi mkubwa katika maendeleo ya kipaumbele hiki na utekelezaji wake miongoni mwa Waadventista....
Ellen White anasema nini kuhusu Maombi?
Je, umewahi kuwa na mzigo ambao ulihitaji kumwambia mtu, lakini uliogopa kuhukumiwa ikiwa ungefanya hivyo?
Ellen G. White au Biblia—Kipi ni Muhimu Zaidi kwa Waadventista?
Biblia—bila shaka—ndiyo kitabu muhimu zaidi. Ni kipimo tunachotumia kupima maandishi mengine yote, ikiwa ni pamoja na yale ya Ellen White.
Ellen G. White Alisaidia Vipi Katika Kuanzisha Kanisa la Waadventista wa Sabato?
Ellen G. White, mwanamke mnyenyekevu kutoka Gorham, Maine, alikuwa mmoja wa waanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato na kiongozi muhimu tangu mwanzo wake.
Ellen White na Kitabu cha Pambano Kuu
Pambano Kuu ni moja ya vitabu vya Ellen G. White vinavyo thaminiwa zaidi na Waadventista wa Sabato.
Roho ya Unabii Ni nini (Kitabu cha 1-4) na Ellen G. White?
Kutumia unabii wa Biblia katika historia, matukio ya hivi karibuni, na hasa siku za usoni, inaweza kuwa kazi ngumu. Hata linaweza kuwa jambo la kutisha kidogo kwa baadhi.
Ellen White Alifundisha nini Kuhusu Matumizi ya Vyakula Vinavyotokana na Mimea?
Moja ya mambo ambayo unaweza kuwa umewahi kusikia kuhusu Waadventista wa Sabato ni msisitizo wao kwenye mtindo wa maisha wa kutumia vyakula vinavyotokana na mimea.

























