Kuelewa Unabii katika Biblia

Waadventista wa Sabato huweka msisitizo mkubwa katika kujifunza unabii.

Kwa kweli, Uadventista una mizizi yake katika kujifunza neno la Mungu, hasa unabii unaohusiana na nyakati zijazo. Na tunashikilia kwamba kuelewa na kutumia unabii wa Biblia kwa usahihi ni muhimu kwa uzoefu bora wa kiroho.

Hebu tuangalie mambo ya msingi kuhusu unabii wa Biblia:

Hebu tuanze na tafsiri.

Unabii wa Biblia unamaanisha nini?

Katika Biblia, unabii unarejelea tu mawasiliano yoyote ya mapenzi ya Mungu kwa wanadamu kupitia mwanadamu. Na cheo cha “nabii” kinamhusu mtu anayepokea na kuwasilisha ujumbe huu kutoka kwa Mungu.

Unabii unaweza kuzungumzia:

Mambo yaliyotokea zamani

 A sign on the beach pointing towards the past and the future

Photo by Hadija on Unsplash

Katika Biblia, aina hizi za unabii zilitolewa kwa madhumuni ya kujifunza kutoka kwenye historia ya watu wa Kiyahudi— mema na mabaya.

Ziliwakumbusha wafuasi wa Mungu yale aliyowafundisha nyakati za kale. Na kama hawakuwa wakifuata mafundisho haya, manabii walishiriki mambo haya ili kuwasaidia kurejea katika njia sahihi—kuishi kulingana na kanuni ambazo Mungu aliwapa kwa ajili ya manufaa yao wenyewe.

Mfano mzuri wa hili unapatikana katika maneno ya nabii Yeremia. Aliwaonya Waisraeli juu ya maangamizi yanayokuja kwa sababu ya kutotii kwao. Aliwaelekeza kwenye “njia za zamani” kama njia yao pekee ya kuokoka. Aliwashauri akisema:

“BWANA asema hivi, Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu” (Yeremia 6:16, SUV).

Tunaweza pia kuangalia nyakati nyingi ambazo Musa alilazimika kuleta ujumbe kutoka kwa Mungu kwa Waisraeli alipokuwa akiwaongoza kwenda Nchi ya Ahadi. Walipoanza kutilia shaka au kujaa hofu, aliwakumbusha yale ambayo Mungu alikuwa amewatendea (Kutoka 15, 16, 17), na Mungu angewapatia tena mahitaji yao.

Maswala ya sasa au ya kisasa

Mungu pia alinena na watu Wake kupitia manabii kuhusu mambo yaliyokuwa yakitokea wakati huo. Wakati mwingine ilikuwa ni kufunua mambo yasiyo julikana yaliyokuwa yakiendelea, au wakati mwingine ilikuwa ni Mungu kuwaita watu wazingatie mambo muhimu.

Kama wakati wa matengenezo ya kidini ya Mfalme Yosia.

Wakati Hilkia Kuhani alipogundua “Kitabu cha Torati katika nyumba ya Bwana,” mfalme alimuuliza nabii mwanamke aitwaye Hulda kuhusu yaliyokuwa yameandikwa humo. Nabii huyo mwanamke aliwapa jibu la moja kwa moja kutoka kwa Mungu kuhusu hatima ya Yuda. Pia alimtia moyo mfalme katika juhudi zake za matangenezo (2 Mambo ya Nyakati 34:14-28, SUV).

Mfano mwingine ni wakati Mfalme Hezekia alihitaji mwongozo juu ya jinsi ya kukabiliana na mzozo wa kisiasa wakati Ashuru ilipotishia kuivamia Yuda. Mungu alimtumia nabii Isaya kumpa uhakikisho wa ulinzi (Isaya 37).

Na pia kuna wakati ambapo Mfalme Daudi alifanya uzinzi na mke wa mmoja wa askari wake. Alipojaribu kuficha kosa hilo kwa kumfanya askari huyo auawe vitani, Mungu alimpelekea Daudi nabii pia.

Nabii Nathani alimwelekeza mfalme kwa busara kuona uzito wa dhambi aliyokuwa ameifanya. Na kutambua haja yake ya kutubu na kumwomba Mungu msamaha (2 Samweli 11,12).

Mambo yatakayokuja kutokea baadaye

Unabii mwingi wa Biblia ulihusu mambo ya baadaye. Kwa kweli, kila tunaposikia kuhusu “unabii” huwa tunauhusisha na ufunuo wa mambo yatakayokuja kutokea baadaye.

Na kuna sababu nzuri nyuma ya mwitikio huu wa haraka.

Biblia imejaa ujumbe kutoka kwa manabii waliotabiri mambo ambayo yangetokea katika siku za usoni za karibu au za mbali.

Hapa kuna aina mbalimbali za unabii wa mambo yajayo:

  • Hatima ya watu binafsi, kama vile Mfalme Yosia na Yohana Mbatizaji
  • Unabii wa Kimasihi (kuhusu Yesu)
  • Hatima ya Israeli kama taifa
  • Yatakayowapata watu wa Mungu katika vizazi vijavyo
  • Matukio ya dunia yajayo jinsi yatakavyotokea katika historia
  • Mwisho wa historia ya dunia na Kurudi kwa Pili kwa Kristo
  • Nini kitatokea baada ya ujio wa pili wa Kristo, na wakati Mungu atakapoumba mbingu mpya na nchi mpya

Na jambo bora zaidi ni kwamba unabii mwingi kati ya huu umetimia kama vile manabii walivyosema ungekuwa.

Kujua hili hutusaidia kuamini Biblia Takatifu kama Neno la kweli la Mungu. Na kuamini kwamba unabii mwingine ambao bado haujatimia pia utatimia kama ulivyotabiriwa wakati wake utakapofika.

Biblia inatuambia kwamba njia ya kumjaribu nabii wa kweli au wa uongo ni kwa kutazama kama unabii wake umetimia. Biblia inasema:

“Atakaponena nabii kwa jina la BWANA, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena BWANA; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope” (Kumbukumbu la Torati 18:22, SUV).

Hivyo, ukweli kwamba unabii wa Biblia umetimia ni ushahidi kwamba unabii wa Biblia umetoka kwa Mungu.

Aina za unabii wa Biblia

Unabii wa Biblia umegawanyika katika makundi kadhaa. Makundi haya hutusaidia kuelewa kwa nini Mungu alitimiza au hakutimiza baadhi ya unabii. Pia hutusaidia tunapotafsiri unabii huu.

Hebu tuyaangalie:

Unabii wenye masharti au usio na masharti

1. Unabii wenye masharti – Huu ni unabii ambao kutimia kwake kunategemea kama watu watatii amri za Mungu au la.

Mungu Mwenyewe aliweka kanuni hii kupitia nabii Yeremia aliposema:

“Wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuung’oa, na kuuvunja, na kuuangamiza; ikiwa taifa lile nililolitaja litageuka, na kuacha maovu yake nitaghairi, nisitende mabaya yale niliyoazimia kuwatenda.

 

Na wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuujenga na kuupanda, ikiwa watatenda maovu mbele za macho yangu, wasiitii sauti yangu, basi nitaghairi, nisitende mema yale niliyoazimia kuwatendea” (Yeremia 18:7-10, SUV).

Utaona mfano mwingine mzuri wa hili katika hadithi ya Yona na mji wa Ninawi (Yona 3:1-10).

Ninawi ulikuwa mji wa ukatili sana. Na Mungu alikuwa ameamua kuuangamiza kama wakazi wake wasingetubu makosa yao na kubadilika ndani ya siku 40. Lakini Yona alipowahubiria na kuwaonya juu ya hatari yao, walijinyenyekeza na kutubu.

Yona 3:10 inatuambia kwamba “Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende” (SUV).

2. Unabii usio na masharti – Unabii ni maelezo ya mambo yajayo. Hayaathiriwi na hali zinazobadilika, na lazima yatimie kama yalivyotabiriwa.

(Na hii inatupa njia ya uhakika ya kutambua mambo haya yanapoanza kutokea, kwa kuwa tutajua maelezo yote lazima yaendane. Mungu hafanyi unabii usio kamili!)

Unabii mwingi kati ya huu unahusiana na hatua muhimu katika Mpango wa Wokovu.

Lazima unabii huu utimie wakati wowote yanapolingana na mpango mkubwa. Hakuna mwanadamu anayeweza kuzuia au kubadilisha unabii huu.

(Hii inajumuisha kuzaliwa kwa Yesu Bethlehemu, kufa kwake msalabani, au Kurudi Kwake Mara ya Pili.)

Yesu alikuja na kufa kwa ajili ya wanadamu ingawa wengi wao hawakumkubali.

Kwa kuwa ilikuwa sehemu ya mpango wa Mungu wa kiungu, ilitokea kama Mungu alivyokuwa anajua itatokea. Na kutokana na hili, tunajua kwamba Atarudi tena wakati wake utakapofika.

Unabii wa mambo yajayo na usio wa mambo yajayo

1. Unabii wa mambo yajayo

An open gate leading to apocalyptic city ruins

Photo by Daniel Lincoln on Unsplash

Huu ni unabii unaozungumzia nyakati za mwisho, au kipindi kabla tu ya Kuja kwa Pili kwa Yesu.

Wakati unabii huu hutumia lugha ya picha, unabii mwingine hutumia lugha ya moja kwa moja na halisi.

Mifano ya lugha ya picha inaweza kupatikana katika vitabu vya Ezekieli, Danieli na Ufunuo.

Danieli 7 na Ufunuo 13 huzungumzia wanyama wenye pembe na taji. Na kuhusu joka na mnyama mwingine anayesujudiwa. Kisha Ufunuo 17 unazungumzia mwanamke aliyekaa juu ya mnyama. Haya yote yanawakilisha matukio na mienendo tofauti ya siku za mwisho na jinsi yanavyowaathiri watu wa Mungu. Na wakati utakapofika, tutaweza kuunganisha mambo haya.

Mfano mzuri wa lugha isiyo ya picha au lugha halisi katika unabii wa nyakati za mwisho unapatikana katika Mathayo 24, Marko 13, na Luka 21.

Kuna pia aya nyingine1 iliyotawanyika katika Agano la Kale na Jipya inayofafanua kuhusu nyakati za mwisho.

[Huenda umewahi kusikia kuhusu “dhiki kuu” itakayokuja mwishoni mwa wakati, wakati dunia itaachwa iendelee kwa mapenzi yake yenyewe. Au labda una maswali kuhusu jinsi Kuja kwa Pili kwa Yesu kutakavyotokea.

Ili kujibu maswali kama haya, hapa kuna somo bora la Biblia linaloshughulikia mambo ya ndani na nje ya unabii huu na mengine zaidi.]

2. Unabii usio wa siku za mwisho

Huu ni unabii wote wa Biblia ambao hauhusu matukio ya mwisho wa wakati kama vile unabii wa kuja kwa Yesu mara ya kwanza kama Masihi, na wa Israeli kama taifa.

Kuna pia unabii wa kwanza kabisa uliotamkwa na Mungu kwa wanadamu, na huo upo katika Mwanzo alipomwambia Adamu na Hawa jinsi hatima ya wanadamu duniani itakavyokuwa, kwa kuwa walikuwa wanaishi katika dunia yenye mema na mabaya (Mwanzo 3).

Kusudi la unabii wa Biblia

Wakati unabii mwingi unazungumzia mambo yajayo, hilo sio lengo kuu la unabii. Lengo kuu ni kutupa tumaini, kutuunganisha na mapenzi ya Mungu, na kututia moyo kufanya mabadiliko yanayofaa katika hali zetu za sasa.

Unabii unatoa taarifa zinazochochea kuchukua hatua zinazofaa.

Hapa kuna njia tano ambazo unabii unaweza kuimarisha imani na kutuchochea kuchukua hatua:

  1. Kuhimiza uvumilivu na tumaini katika hali ngumu

Waisraeli walipokuwa utumwani Babeli, walikata tamaa na kujiuliza ni lini wataweza kurudi katika nchi yao.

Kisha Mungu akamtuma nabii Yeremia kwao na ujumbe wa kutia moyo katika Yeremia 29. Aliwaambia kwamba ingawa walikuwa na miaka 70 zaidi Babeli, hawakupaswa kukata tamaa.

Mungu aliwahakikishia kwamba mwishowe, angewarejesha katika nchi yao. Neno lake kwao lilikuwa:

“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho” (Yeremia 29:11, SUV).

  1. Kuhamasisha badiliko la moyo

Tunaweza kuangalia katika kitabu cha Danieli kwa mfano mzuri wa hili.

Lengo kuu la unabii wa sura ya 4 lilikuwa kumwongoza mfalme mwenye kiburi “ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini” (Danieli 4:27, SUV).

Ingawa ilichukua muda mrefu na uzoefu mgumu, kiburi cha Nebukadneza hatimaye kilishushwa.

Naye alikiri kwamba Mungu ni mkuu na anaweza kuwashusha wenye kiburi (Danieli 4:37).

  1. Kuonya watu juu ya maangamizi yajayo kutokana na dhambi

Mfano wa hili ni hadithi ya Yona na mji wa Ninawi ambayo tuliangalia awali (Yona 3).
Kwa sababu watu walitubu, waliokolewa na kuepuka kupitia matatizo makubwa. Matatizo ambayo yangewapata ndani ya siku 40 kama wasingetubu.

  1. Kufunua taarifa au kutoa hekima

Katika baadhi ya hali katika Biblia, watu walikutana na ndoto za ajabu, ujumbe wa kuchanganya, au hali za kutatanisha. Mungu alifunua maana ya mambo haya kwa manabii Wake ili waweze kutoa mwongozo kwa watu Wake, au kuonyesha nguvu Zake kwa wapinzani Wake waliotishia watu Wake.

Tunaweza tena kuangalia katika kitabu cha Danieli.

Danieli alikuwa mfungwa wa Israeli huko Babeli. Lakini kutokana na tabia yake njema, alikuwa anafanya kazi katika ikulu ya kifalme. Hivyo, wakati Mfalme Nebukadneza alipoota ndoto ya kutisha, na hakuna “wenye hekima” wake wa kawaida aliyeweza kuelewa ndoto hiyo, Danieli alijitokeza.

Danieli alimpa Mungu utukufu, ambaye alimwomba ampe hekima kuhusu ndoto ya mfalme. Mungu alipompatia, mfalme alishuhudia nguvu za Mungu na akampandisha cheo Danieli (Danieli 2).

  1. Kuruhusu maandalizi kwa ajili ya siku za usoni

Tunakutana hali kama hii wakati Mungu alimwambia Yusufu amwelekeze Farao wa Misri ahifadhi chakula kwa ajili ya njaa ambayo ingekuja miaka kadhaa baadaye (Mwanzo 41).

  1. Kutoa mwelekeo/ufahamu kuhusu hali fulani

Kuna mfano wa hili katika uzoefu wa watu wa Yuda waliorejea Yerusalemu kutoka Babeli.

Walipolegea baada ya muda na kuacha kazi ya kujenga upya Yerusalemu, Mungu aliwatuma manabii Hagai na Zekaria (Ezra 5:1).

Wawili hawa waliwatia moyo wachukue hatua. Na waliwaelekeza kwenye tumaini la Masihi katika siku za usoni.

Kutumia yale tunayojifunza kutoka kwenye unabii

A man carries a leather satchel and Bible on his journey to spread the Gospel.

Photo by Ben White on Unsplash

Kama tulivyoona hapa, kuna unabii mwingi muhimu katika Maandiko. Na kwa kuuchunguza, tunaweza kujifunza masomo muhimu na kuyatumia katika maisha yetu.

Neno la unabii, hata tunaposoma yale yaliyosemwa kuhusu matukio ya zamani, linaweza kutusaidia kujiandaa kwa ajili ya siku zetu zijazo. Kama vile ilivyowasaidia watu ambao lilikuwa limelengwa kwao.

Tunapoona mpango wa Mungu na upendo wake kwa watu wake, tunaweza kumtumaini na maisha yetu. Na tunaweza kumkaribia zaidi.

Pia, tunaweza kujifunza kutokana na makosa ya wengine waliokataa kusikiliza maonyo yaliyotolewa kupitia unabii.

Na la muhimu zaidi, tunaweza kujiandaa kwa ajili ya Ujio wa Pili wa Kristo.

Akirejelea maarifa tuliyonayo kupitia unabii wa siku za mwisho, Petro anatuhimiza akisema:

“Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu” (2 Petro 3:14,17, SUV).

Pia, mbali na kujiandaa sisi wenyewe kuwa tayari Yesu atakapokuja, tunaweza kuwasaidia wengine wawe tayari pia.

Tunawezaje kufanya hivyo?

Kwa kushiriki Injili na kweli tunazozijua pamoja nao.

Kwa kweli, Yesu alitabiri kwamba hili litakuwa moja ya dalili za mwisho.

Alisema kwamba hii “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja” (Mathayo 24:14, SUV).

Umeona hilo?

Kwa kweli, hili ndilo ishara moja inayopingana na zile nyingine za kutisha.

Kwa sababu inaleta tumaini wakati wa kukata tamaa.

Inachochea upendo badala ya chuki.

Inatuchochea kuwafikia wengine kwa hamu ya kuwasaidia na kuungana nao.

Hasa katika dunia yenye maumivu na kifo, inatoa amani na uzima wa milele kwa yeyote atakayekubali na kumwamini Yesu (Yohana 3:16).
Hivyo, hatimaye, kushiriki Injili kunatupa fursa ya kuwa sehemu ya jambo kubwa kuliko sisi wenyewe. Jambo la milele. Jambo la ajabu.

Na huhitaji kuwa mchungaji au msomi wa Biblia kufanya hivi. Kushiriki tu kile ambacho umejifunza hadi sasa, na uzoefu wako wa kumjua Yesu kama Mwokozi na Rafiki yako ni mahali pazuri pa kuanzia.

Kwa nini unabii una maana kubwa kwa Waadventista?

Waadventista wanathamini sana kujifunza unabii wa Biblia kwa sababu kuu kadhaa:

  1. Ndicho kilichoongoza kuanzishwa kwa Kanisa la Waadventista Wasabato.
Biblical Book of the prophet Daniel as Adventist Evangelist delivers his sermon in an Evangelistic series on Bible prophecy

Photo by Ben White on Unsplash

Mwishoni mwa miaka ya 1790, waumini wengine waliona kwamba unabii wa Biblia ulionyesha kurudi kwa Yesu kunakaribia. Na hii ilikuwa tofauti na imani iliyokuwa maarufu wakati huo, ambayo ilichukulia Ujio wa Yesu Mara ya Pili kama tukio la mfano au la kiroho tu (badala ya kuwa linaloonekana au halisi). Kwa wale waliokuwa wanaamini kwamba lingetokea kweli, walitarajia lingekuwa mbali sana, sana katika siku za usoni.

Baada ya kutambua hili, walianza kuhubiri na kuwaambia wengine kuhusu jambo hilo. Watu wengi zaidi walianza kujifunza Biblia zao majumbani mwao, badala ya kusikiliza tu wahubiri wa kanisani wakizungumza juu yake.

Hili liliendelea na kuwa Harakati ya Wafuasi wa Miller nchini Marekani katika miongo ya kwanza ya miaka ya 1800.

Watu kadhaa wenye ushawishi katika harakati hii walikosea kwa kujaribu kuweka tarehe ya Ujio wa Pili wa Kristo, jambo ambalo Biblia inasema tusifanye. Hii ilisababisha Tukio la Kukatishwa Tamaa Kuu mwaka 1844.

Lakini badala ya kupoteza imani yao, idadi kubwa ya hawa wanafunzi wa Biblia wenye bidii walirudi tena kujifunza unabii. Na hapo ndipo walipogundua walipokosea katika tafsiri yao ya Danieli 8:14.

Waliendelea na masomo haya, ambayo yaliwawezesha kujifunza kweli nyingine nyingi za ajabu ambazo Biblia inatoa. Mambo mengi kati ya haya hayakuwa yakisomwa au kutajwa sana katika makanisa ya wakati huo, hivyo kweli hizi zikawa mafundisho ya kipekee ya Waadventista—kama vile Ujumbe wa Patakatifu na Sabato ya siku ya saba.

Hata leo, Waadventista wanahisi kwamba msisitizo juu ya unabii unapaswa kuwa sehemu kuu ya maisha bora ya kiroho.

  1. Unatusaidia kuelewa tabia ya upendo ya Mungu.

Kupitia unabii, tunaona ambavyo katika upendo wake kwetu, Mungu bado ana mamlaka ya mwisho juu ya yote yanayotokea katika maisha yetu na duniani.

Na tunaposoma visa kama vile vya Mfalme Koreshi na Yosia, tunaweza kutia moyo kwamba hata kama dunia imejaa machafuko karibu nasi, Yeye ana mpango kwa kila mmoja wetu. Na tunaweza kupumzika kwa uhakika kwamba mwishowe, kila kitu kitaishia kwa ushindi Wake.

  1. Kujifunza unabii wa Biblia kunatupa mtazamo wa kipekee maishani
Person studying the Biblical prophecies and taking notes as it provides us unique perspective in life and in world history.

Photo by Fa Barboza on Unsplash

Tunaweza kuona picha kubwa katika hali mbalimbali za maisha yetu binafsi au hata matukio ya dunia na historia.

Unatufunulia kwamba mambo sio kila mara yako kama yanavyoonekana. Mara nyingi, mambo mabaya au yanayochanganya yanayotokea duniani wakati wowote hayalingani na jinsi Mungu atakavyorekebisha kila kitu siku moja.

Na unatukumbusha kwamba kuna nguvu za kiroho zinazofanya kazi nyuma ya pazia. Hatuwezi kila mara kuwaamini wanadamu. Ni Mungu pekee.

Hivyo tena tunaweza kushikilia uhakika kwamba Mungu siku zote anafanya kazi kuhakikisha wokovu wetu. Kwamba Yeye siku zote anafanya kazi kutulinda dhidi ya hatari na kututia moyo katika njia salama.

Ndiyo maana mada ya unabii wa Biblia haitupaswi kututia hofu. Badala yake tunaweza kupata faraja ya kina tukijua kwamba haijalishi dunia hii itaingia katika hali gani, Mungu atabaki nasi daima na atashinda mwishowe.

Unabii wote unaelekeza kwenye ushindi wa Yesu kwa ajili yetu. Ushindi dhidi ya dhambi, kifo na mateso atakaporudi katika Kurudi Kwake Mara ya Pili.

Jifunze zaidi kuhusu manabii waliotoa unabii huu wa Biblia.

Chagua Masomo ya Biblia Mtandaoni

Unataka kuendelea kujifunza? Pata habari zaidi kuhusu Yesu, mwanadamu, mpango wa wokovu, na jinsi Mungu anavyokupenda kiasi cha kutosha kujitolea kila kitu, ili tu kukupatia nafasi ya kumchagua.

Wakati mwingine inaweza kuwa ngumu kujua pa kuanzia, ndio maana tunatoa chaguo za masomo ya Biblia mtandaoni bure, rahisi kutumia, unaweza kufanya wakati wowote, mahali popote, na kwa kasi yako mwenyewe.

Shule hii ya Biblia mtandaoni itakuelekeza kupitia mada kuu za Maandiko, ikivunja dhana ngumu za Biblia katika vipande vidogo, ambavyo vinaweza kukusaidia kupata majibu ya maswali magumu zaidi ya maisha.

  1. Revelation 5:12; 7:17; 17:14 []

Makala Zinazohusiana

Je, Una swali kuhusu Waadventista? Uliza hapa!

Pata majibu kwa maswali yako kuhusu Waadventista Wasabato

Majibu Zaidi

Kuna Historia Gani Nyuma ya Biblia? Muhtasari Kamili

Kuna Historia Gani Nyuma ya Biblia? Muhtasari Kamili

Kuna Historia Gani Nyuma ya Biblia? Muhtasari KamiliBiblia ni kitabu ambacho kimeuzwa zaidi duniani wakati wote.1 Imetafsiriwa katika maelfu ya lugha, kusomwa na watu wa umri na asili mbalimbali. Ukubwa wake ni wa kipekee. Lakini ni nini historia ya Biblia? Hiyo pia...